Zahara Muhidin Michuzi akiweka sahihi katika kitabu cha wageni alipowasili katika ofisi za CCM mkoa wa Tabora ili kuchukua form ya kugombea viti maalum kwa vijana.
Binti huyo wa Michuzi mara baada ya kuhitimu elimu yake ya shahada yake ya uchumi UDOM ameona ni vyema akawatumikia wananchi wa nyumbani kwake mkoani Tabora kwa kutangaza nia ya kugombea ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
 Zahara Michuzi (kushoto) na Mwasham Hashim (kulia) karani wa UVCCM Tabora akitoa maelekezo ya uchukuaji wa form hizo.
 Zahara Michuzi akikabidhiwa form yake leo katika ofisi za UVCCM mkoa-Tabora
 Zahara akiifurahia form yake ya Ubunge wa viti maalum Tabora.
 Zahara (kushoto) akilipia fedha  ya form hiyo huku mama yake mlezi, Rehema Saidi (katikati),  akishuhudia kitendo hicho. Picha na Aloyson Blog wa TBN kanda ya Magharibi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 16, 2015

    The mdudu, hongera sana mjomba Michuzi kumbe una kabinti? sasa kama kaamua kugombea wala msijisumbue kupiga kampeni maana huyo ashapita bila ya kupingwa hana mpinzani,,,, ila mm The mdudu nishahama vyama vyote na nimehamia ACT Wazalendo nimevutiwa na AZIMIO LA TABORA + LA ARUSHA na hao kanjibai fisadiz watafute pakukimbilia maana nnausongo nao ile mbaya.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 16, 2015

    HIYO NIMEIPENDA,NITAKUJA KUMPIGIA KAMPENI HUYO.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 16, 2015

    Tunakutakia heri njema mama ushinde.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 16, 2015

    Kumbe Michuzi wa kukaya? kila la kheri kwa mwanao.

    ReplyDelete
  5. Hongera Sana Zahara...uongozi upo nafsini mwako,natumai utafanya vyema kama ulivyofanya vyema kwenye uwakilishi kama huo Chuoni!!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 16, 2015

    SALUTE MJOMBA KWA KUKUZA. Lakini dukuduku langu ni hizi siasa za bongo ambazo nitafurahi kama wadau watanisaidia? Nimenotice watu wanakurupuka na kuchagua sehemu za kugombea bila kigezo muhimu cha UKAZI WA LILE ENEO FOR A CERTAIN PERIOD OF TIME. Sifahamu kigezo cha NEC kinataka uwe na hiyo address kwa muda gani kabla haujaitwa mkazi. Miss Tanzania ndio waliokuwa wanaitumia hii style kwa kuwaallocate wasichana wazuri kwenye maeneo mbalimbali just to qualify them kwa final. Kama huu utamaduni unaachwa uingie kwenye siasa, then sisi REALLY wenyeji wa huku songombingo tumeisha. Mungu Mpenzi uturehemu.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 17, 2015

    Twamtakia Binti yetu kila la kheri. Aidha hongereni wote kwa malezi mema.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...