KIKOSI cha timu ya Friends Rangers, kesho asubuhi kinashuka kwenye Uwanja wa Azam Complex, uliopo Chamazi Dar es Salaam, kuvaana na timu ya Azam FC, katika mchezo wa kirafiki.

Ofisa habari wa klabu hiyo Asha Kigundula, alisema kuwa mchezo huo utafanyika asubuhi kuanzia saa 2, asubuhi.

Kigundula alisema kuwa wameshukuru kupata mechi hiyo ambayo itaendelea kuiweka timu yao katika mazingira mazuri kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi daraja la kwanza.

Alisema kuwa kucheza na timu kama Azam ni sehemu nzuri ya kukipa kikosi chao mazoezi mazuri, kwa sababu Azam ni timu bora na inawachezaji wenye uwezo mkubwa hapa nchini.

Kigundula alisema tayari kikosi chao kimeshacheza mechi mbili za kirafiki, dhidi ya Yanga ambapo ilifungwa mabao 3-2, mchezo uliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume, Ilala Dar es Salaam.

Mechi nyingi ambayo Friends Rangers ilicheza na timu ya Mwadui, ambapo timu hiyo ya Magomeni Kagera ilishinda mabao 2-1.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...