Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, akisalimiana na Bi. Jackline Maleko, Mkurugenzi Mtendaji wa TANTRADE  alipowasili viwanjani hapo kutembelea Maonesho ya 39 ya Biashara ya kimataifa mapema. Mahakama ya Tanzania inashiriki katika Maonesho ya Sabasaba lengo likiwa ni kutoa elimu kwa wananchi juu ya taratibu na huduma mbalimbali zinazotolewa. Katika Banda la Mahakama kuna uwakilishi wa Mahakama za Mwanzo, Wilaya, Mkoa/Hakimu Mkazi, Mahakama Kuu, Mahakama ya Rufani, Tume ya Utumishi wa Mahakama pamoja na Tume ya Kurekebisha Sheria.

 Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, akipata maelezo kutoka kwa Bw. Machumu Essaba, Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), Mahakama jinsi mfumo wa JSDS unavyofanya kazi Mahakamani. Maelezo hayo yalitolewa pindi Mhe. Jaji Mkuu alipotembelea banda la Mahakama ya Tanzania. Pembeni ya Mhe. Jaji Mkuu ni Mhe. Shaban Ally Lila, Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
 Mhe.Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, akipata maelezo kuhusiana na Mahakama ya Rufani (T) kutoka kwa Mhe. Phocus Bampikya, Naibu Msajili Mwandamizi, Mahakama ya Rufani (

 Mhe. Jaji Mkuu akipata maelezo kutoka kwa Afisa wa Polisi alipotembelea banda la Polisi katika ziara yake uwanjani hapo. 
1.   Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikati), akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) alipotembelea Banda la Mahakama ya Tanzania, kushoto ni Mhe. Shaban Ally Lila, Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kulia ni Bw. Edwin Rutageruka, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara (TANTRADE), katika mkutano huo na Waandishi wa Habari, Mhe. Jaji Mkuu alieleza juu ya mikakati mbalimbali ambayo Mahakama inayo yenye lengo la kuboresha huduma ya utoaji haki nchini na kuwataka wananchi kutembelea banda la Mahakama ili kupata elimu hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...