Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Mkuu wa Utawala, Bi Lilian Munanka, ambaye Balozi amemwelezea kama Afisa Mkuu Mwandamizi, mweledi, mchakapakazi, anayejituma na mwajibikaji, mwenyeuzoefu mkubwa na nguzo ya kutegemewa na ambaye amewapokea Mabalozi wengi.
Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akiwa na baadhi ya maafisa na wafanyakazi wa Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa wakiongonzwa na Balozi Ramadhani Mwinyi.

Katibu Mkuu, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, amewaaga watanzania waishio nchini  Marekani,  kwa kuwataka kujivunia utanzania wao na kutoionea aibu lugha yao ya taifa,   Kiswahili.

Mwishoni mwa wiki,   Ubalozi wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania nchini Marekani,  uliandaa hafla ya aina yake  ya  kumpongeza, kumshukuru na kumuaga  Balozi Liberata  Mulamula ambaye sasa ni  Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Hafla hiyo iliyowajumuisha  watanzania wa kada mbalimbali wakiwamo maafisa na  wafanyakazi wa Uwakilishi wa Kudumu wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, wakiongozwa na   Balozi  Ramadhan  Mwinyi,  ilipambazwa kwa nasaha mbalimbali na salamu za kumtakia kheri Balozi Mulamula katika  jukumu lake jipya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 29, 2015

    Hakuna anaeona aibu kuongea kiswahili kwani ndiyo lugha ya kwanza kwa umaarufu africa nzima.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...