Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Business Connexion,Seronga Wangwe akizungumza katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Hayatt Regence jijini Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi mkuu mtendajiwa Kampuni ya Business Connexion, Issac Mophallene akizungumza katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Hayatt Regence jijini Dar es Salaam leo.
Afisa Uendeshaji Mkuu katika Kampuni la Business Connexion, Jane Canny akizungumza katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Hayatt Regence jijini Dar es Salaam leo.
 Mwandishi wa habari wa gazeti la The African, Jastine Amani akiuliza swali kuhusiana na utendaji kazi wa mitandao ya simu hapa nchini katika
mkutano uliofanyika katika hoteli ya Hayatt Regence jijini Dar es Salaam leo.Kushoto ni mwandishi wa habari wa gazeti la The Gurdian, Frenk Amani.

MUDA UMEFIKA WA KUPANUA BIASHARA TANZANIA
TANZANIA ina fursa nyingi ambazo bado hazijatumika. Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, uchumi unategemewa kukua kwa wastani wa asilimia7.2 mwaka huu na uwekezaji wa serikali kwa kiasi kikubwa katika mkongo wa taifa unaongeza biashara na upatikanaji wa teknolojia kwa raia ili kujenga fursa za kusonga mbele kwenye teknolojia zetu. Pamoja na kuibuka kwa teknolojia nyingi zisizokuwa na mpangilio, hatua hii imewekwa kwa ajili ya kuongezeka kwa fursa nyingi. Haya ni maoni ya Jane Canny, Afisa Uendeshaji Mkuu katika Kampuni la Business Connexion.
Kampuni ya business Connexion Tanzania imekuwa ikifanya kazi tangu mwaka 2000, lengo lake kubwa hasa ni kujikita katika huduma za kifedha, mawasiliano ya simu, nishati na madini na sekta ya umma. Kupitia matumizi bunifu ya teknolojia na ushirikiano wetu na UmojaSwitch Consortium, Tunatoa huduma ya upatikanaji wa miundombinu ya malipo iliyo salama katika benki 28 na mashine za ATM 200 nchini Tanzania. Miundombinu hii imeunganishwa na swichi tano za malipo ndani ya Afrika Mashariki ili kuruhusu miamala ya kimataifa, makampuni makubwa matatu ya mitandao ya simu ili kuwezesha malipo ya simu na taasisi mbalimbali za serikali katika kuwezesha makusanyo ya malipo ya kielektroniki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...