Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam imetiliana saini  mkataba wa mashirikiano ya kusaidiana na jiji la Hamburg la Ujerumani. Mkataba huo umesainiwa leo na Mstahiki Meya wa Kinondoni Mhe. Yusuf Mwenda na State Secretary wa Hamburg, Bw. Wolfgang Schmidt, ambapo  kutajengwa mtambo wa kisasa wa kuchakata taka za ugani na kuzalishwa mbolea eneo la Mabwepande wenye thamani ya shilingi za kitanzania ni bilioni 3.5 ambazo zitatolewa na jiji la Hamburg.
Mstahiki Meya alisema ukishajengwa mtambo huu sio tu Kinondoni itakuwa safi bali pia  ajira 1000 zitatengenezwa na pia  mbolea nyingi itapatikana na itatumika kwa faida ya kilimo.
Mstahiki Meya wa Kinondoni Mhe. Yusuf Mwenda na State Secretary wa Hamburg, Bw. Wolfgang Schmidt, wakipeana mikono baada ya kusaini mkataba wa mashirikiano ya kusaidiana na jiji la Hamburg la Ujerumani. Kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Eng.Mussa Natty.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...