Je umekwishawahi kukwama kwenye foleni ukajutia kutobeba gazeti walau likusaidie kusogeza muda mbele? Je umekwisha wahi kutafuta chanzo cha habari za uhakika kwenye simu yako ukakikosa?

Je umekwishawahi kuambiwa kuna tangazo la kazi au tenda ila ukashindwa kuliona kwa vile lipo kwenye gazeti la siku za nyuma?
Je umeshawahi kulazimika kuchoma au kutupa magazeti ya siku za nyuma kwa sababu yamejaa sana nyumbani kwako? Au je umeshawahi kuhisi kuna umuhimu wa kuona watoto wako wanachojifunza shuleni?

Je umekwishaona maktaba inayokupa magazeti, majarida au vitabu vyote toka tulipopata uhuru, mahali popote wakati wowote ulipo?

Kama jibu la swali lolote kati ya hayo ni ndio, basi M-Paper inaweza kukupa hayo yote.

Kabla hatujaendelea, tazam video hii ya sekunde thelathini tu  https://www.youtube.com/watch?v=x00FXMqY-jg

M-Paper ni programu ya simu za mkononi, inayokuletea magazeti, majarida na vitabu vyote kwenye simu yako ya mkononi.  Programu hii ya kipekee itakufanya usome gazeti, jarida au kitabu chote kama kilivyo kwenye makaratasi na si vichwa vya habari pekee.

Kama hiyo haitoshi, watengenezeji wa programu hii watakupa shilingi 10,000 pale utakapodownload app hii ambayo utaitumia kununua magazeti, vitabu na majarida kabla hujaanza kutumia pesa zako.

Oh, jambo jingine la kipekee kuhusu program hii ni kuwa, magazeti, majarida na vitabu vyote vinauzwa kwa nusu bei. Faida mara mbili.




Unaweza kudownload app hii hapa http://www.mpaper.co.tz kisha ukaniandikia maoni yako hapa chini, umeionaje? Kumbuka unadownload BURE, unawekewa 10,000 kwenye akaunti yako hivyo huna cha kupoteza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ankiln MosesJuly 28, 2015

    Safi sana Mzee,

    Hii itatufaa sana sisi watu wa ughaibuni, maana tunapitwa na habari + matangazo ya magezitini kama tender na vinginevyo.

    Hongereni wakuu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...