Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL) Roberto Jarrin (kushoto) akisalimiana na Mhariri Mkuu wa kampuni ya magazeti ya serikali ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayochapisha magazeti ya Daily News ,Habari Leo na Spoti Leo,Bw.Gabriel Nderumaki(wa pili kulia) alipofanya ziara ya kutembelea ofisi hizo zilizopo eneo la Tazara barabara ya Sam Nujoma jijini Dar es Salaam, wengine pichani wa kwanza kushoto ni Afisa Uhusiano wa TBL Emma Oriyo aliyesimama nyuma kulia ni Meneja wa Media wa kampuni ya Aggrey&Clifford Bw.Oliver Mutere.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL) Roberto Jarrin (kushoto) akibadilishana mawazo na Mhariri Mkuu wa kampuni ya magazeti ya serikali ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayochapisha magazeti ya Daily News ,Habari Leo na Spoti Leo,Bw.Gabriel Nderumaki(kulia) alipofanya ziara ya kutembelea ofisi hizo zilizopo eneo la Tazara barabara ya Sam Nujoma.
Ujumbe wa TBL ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Roberto Jarrin katika mazungumzo na watendaji waandamizi wa kampuni ya Tanzania Standard wakiongozwa na Mhariri Mtendaji Gabriel Nderumaki.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Breweries Limited (TBL) Roberto Jarrin (Kushoto) akitembezwa katika eneo la ofisi za kampuni ya Mwananchi Communications na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Bwana Francis Nanai (kulia) alipofanya ziara kwenye ofisi za kampuni hiyo zilizopo Mabibo Relini jijini Dar es Salaam wengine kwa nyuma ni Maofisa waandamizi wa kampuni ya Mwananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...