Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) linatarajia kutoa shilingi milioni 700 kwa Benki ya Posta Tanzania kama dhamana ya mikopo itakayotolewa na benki hiyo kwa wajasiriamali hapa nchni.
Mpango huu uko chini ya Mfuko wa Taifa wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ulioanzishwa mwaka 2008 ambao pamoja na majukumu mengine unatumika kutoa au kudhamini mikopo yenye masharti nafuu kwa wajasiriamali nchini.
Fedha hizo zitawekwa katika akaunti maalum katika Benki ya Posta kama dhamana ya mikopo na benki hiyo itatumia fedha zake kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa makundi husika kwa kiwango cha mara tatu ya dhamana iliyowekwa na Baraza.
Mikopo itatolewa kwa riba ya asilimia 11 kwa mwaka.
“Tunaanza na Benki ya Posta na baadae nyingine zitakazofanya kazi na sisi, utekelezaji unaanza mara moja kwanza na kiwango hiki cha fedha ambacho kitaongezeka,” alisema.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...