Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala akimkabidhi Rais Dkt .Jakaya Mrisho Kikwete cheti cha Shahada ya Heshima ya Doctor of Laws(Honoris Causa) wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi Rais joho na cheti iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na maprofesa waandamizi wa chuo hicho.Tayari Rais Kikwete alishatunukiwa shahada hiyo katika mahafali ya 41 ya UDSM yaliyofanyika Octoba mwaka 2011.
Profesa Agnes Mwakaje wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akimvika kofia ya kitaaluma Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi Rasmi Rais Joho na cheti cha shahada ya heshima ya Doctor of Laws(Honoris Causa) ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala akisoma maelezo mafupi baada yeye na jopo la maprofesa waandamizi wa chuo hicho kumkabidho Joho la taaluma na cheti cha Shahada ya heshima ya Doctor of Laws(Honoris Causa) ya chu kikuu cha Dar es Salaam wakati wa hafla iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandakla pamoja na maprofesa waandamizi wa chuo hicho muda mfupi baada hafla fupi ya kumkabidhi Rais Joho na Cheti cha Shahada ya Heshima ya Doctor of Laws(Honoris Causa) ikliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo(picha na Freddy Maro)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 21, 2015

    Hongera Mheshimiwa raisi kwa shahada hii ya heshima ya udaktari wa sheria.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 21, 2015

    Congratulation.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 22, 2015

    REALLY? DILI NZURI YA KUINGIA IKULU. ANDAENI JOHO LINGINE LA MHESHIMIWA MAGUFULI

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 22, 2015

    Hongera Mh Rais

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 22, 2015

    Siasa bwana!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...