Uongozi wa Kampuni ya
Reli Tanzania –TRL unasikitika kuwataarifu wananchi na abiria waliokuwa
wasafiri na treni ya leo Ijumaa Julai 24, 2015 kutoka Dar es Salaam kwenda bara
kuwa safari hiyo imeahirishwa hadi kesho saa 11 jioni.
Kwa mujibu wa taarifa
hiyo sababu za kuahirishwa safari hiyo ni ajali ya treni ya mizigo iliyotokea
leo Ijumaa Julai 24, 2015 saa 8:15 alasiri
maeneo ya Stesheni za Mazimbu –Mkata mkoani Morogoro ambapo ilihusisha mabehewa matano ya
treni ya
mizigo iliyokuwa inasafiri kwenda Bara, manne yaliacha njia na moja kuanguka kabisa.
Tayari Wahandisi wa TRL
wako eneo la ajali kufanya tathmini na
kuanza zoezi la uokoaji, ikiwemo kazi ya
kuyanyanyua mabehewa yaliyopata ajali na kisha kukarabati njia ili iwezwe
kupitika mapema hapo kesho.
Uongozi
wa TRL inawaomba radhi wananchi na wateja wake wote nchini kwa usumbufu utakaojitokeza.
-Tamati-
Imetolewa na
Afisi ya Uhusiano ya TRL kwa Niaba ya
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ,
Mhandisi Elias Mshana
Dar es
Salaam,
Julai 24, 2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...