Waandishi wa Vyombo mbali mbali vya habari nchini Tanzania na nje walioweka kambi kwenye Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma kwa ajili ya kutoa taarifa za vikao mbali mbali vinavyopendelea ili kumpata mgombea Urais wa Mwaka 2015 kupitia chama hicho.
UPDATES:  Kikao cha  Kamati Kuu ya CCM   kimemalizika hapa Dodoma na Nape Nnauye akiongea na wanahabari hivi punde amesema kikao kimaeenda vyema kabisa na kumalizika vizuri - ila majina hatoyataja sasa. Hadi kesho saa nne asubuhi.... 
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete(wa pili kushoto) akiongoza kikao cha Kamati Kuu Maalum cha CCM mjini Dodoma, Kikao hicho kitachuja majina ya wagombea na kupata majina matano(5) .
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa taarifa fupi ya wajumbe waliohudhuria kikao cha Kamati Kuu Maalum ambapo wajumbe 28 walihudhuria kati ya 32.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakipitia baadhi ya makabrasha wakati wa kikao cha Kamati Kuu Maalum (Picha na Adam Mzee)

Vijana wa CCM wakipakia mikoba yenye makabrasha ya mkutano maalum wa CCM Taifa 2015 unaotarajiwa kuanza baadaye leo  katika ukumbi mpya wa Dodoma Convention Centre mjini Dodoma  uliozinduliwa juzi.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 10, 2015

    Hello Michuzi tunakutegemea sana hasa mashariki ya mbali.....Chennai India. Tupo huku kwa libeneke la raha zetu. Endelea bila wasi kutupa breaking news za matokeo ya CCM hapo Dom.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 10, 2015

    Mbona updates hazibadiliki Michuzi? Tujuze nini kinaendelea mkuu.tunakutegemea

    ReplyDelete
  3. Ni lowasa Tu ndio anapita

    ReplyDelete
  4. Kazi nzuri Michuzi, kinachotia raha Ni uwezo wako wa kutoa taarifa sahihi. Hongera Sana naana Ni wazi mchakato wa CCM kwa 99% ndiyo unamtoa Rais!!

    ReplyDelete
  5. Tuwe Waungwana....Michuzi anatoa anachopewa.....apike data!!!! Tutulie.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 10, 2015

    Jagular umebebeshwa LUMBESA?? Muogopeni Maulana jamani eh!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 10, 2015

    Ni Magufuli ndio atateuliwa.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 10, 2015

    Ni Magufli ndio atakaepita.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 11, 2015

    Naungana na huyo anaekisia kuwa Magufuli ndiye atakayepita kwa sababu Magufuli ni mchapakazi na hana mzaha na mtu. Kama vile vile kila Wizara aliyopewa alifanya vizuri sana basi hata akifaulu kuwa Rais wa nchi yetu most likely ni kwamba wembe wake utakuwa ni ule ule na hata kupita.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 11, 2015

    Magufuli hafai ubabe mwingi sana tunataka kiongozi mpole na mstaarabu kama lowasa au bilal

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 11, 2015

    hello michuzi

    pole kwa majukumu

    Hapa mambo hayaendi kazi haifanyiki wapeznzi wa siasa tunataka upadates toka dodoma yaani toka majira ya saa mbili tupo online kuona lolote ila kimya atleast tumepata update saa sita tafadhali tunaomba update angalao tuendelee na kazi za mwekezaji!!!!duuuu
    kazi hazifanyiki huku asubuhi mbali kiu ya kujua ndo imepanda saaana

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 11, 2015

    Majina ni lowasa, Asha migiro,Bilal, Membe na Magufuli. Na kinyangiro ni Kati ya Lowasa na Asha Migiro.

    ReplyDelete
  13. Majina yanatolewa leo saa nne ya asubui
    So stay tunned na pia yatarushwa moja kwa moja kwenye radio

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 11, 2015

    Majina yanatajwa kesho asubui

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 11, 2015

    Majina yaliyppitishwa ni:
    1. Bernad Membe
    2.John Pombe Magufuli
    3. Asha Rose Migiro
    4. January Makamba
    5.Amina Ali Salum

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 11, 2015

    Ccm tangazeni majina munaogopa nini? Mara hii ndio kifo chenu mukichemsha kuweka mgombea mzuri mumekwisha

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...