Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ,Jasper Mero akizungumza katika mkutano wa Wadau wa Kujadili mpango mkakati wa  miaka mitano wa ofisi ya CAG uliofanyika leo jijini Dar es Salaam 
Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ,Jasper Mero  (mwenye tai katikat)akiwa katika picha ya pamoja na wadau kujadili mpango mkakati wa miaka mitano wa ofisi ya CAG uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jami.
 
Imeelezwa kuwa kufikia mlaengo kwa ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inategemea na mchango wa wadau mbalimbali katika kupanga mikakati ya kuweza ofisi ya CAG kusimamia pamoja na kutekeleza.
 
Hayo ameyasema leo,Kaimu Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),Jasper Mero wakati akifungua mkutano wa wadau wa kuandaa mikakati ya  Ofisi  ya CAG ya 2016 -2021 katika kuweza ofisi hiyto iweze kusimamia mikakati hiyo.
 
Amesema wadau wametakiwa kutoa maoni kwa uhuru katika ofisi hiyo iweze kupata mikakati ya kuweza kusimamia katika udhibiti wa fedha ya Umma.
 
Mero amesema mikakati ya 2011hadi 2016 imetekekelezwa kwa asilimia 100 hiyo ikiwa imetokana na mahusiano ya ofisi ya CAG pamoja na wadau ambao walitoa maoni chanya katika ofisi hiyo.
 


Amesema katika ofisi ya CAG imepata mafanikio ikiwa ni pamoja kutoa ripoti za mara kwa mara pamoja na kutoa ushauri wa kiutekelezaji kutokana na ukaguzi walioufanya katika mashirika ya Umma ,pamoja na Taasisi za Serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...