Na John Nditi, Morogoro

MKUU wa Mkoa wa Morogoro pichani kati, Dk Rajab Rutengwe, amewaomba  wanawake kuanzia ngazi ya mitaa, vitongoji,  vijiji na kata  kushiriki katika suala la ulinzi shirikishi kwa  kuwafichua wahalifu  wanaotishia kuhatarisha uvujifu wa amani ndani ya  mkoa.

Dk Rutengwe alitoa rai hiyo wakati alipozungumza na wajumbe wa mkutano mkuu maalumu wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Morogoro , Julai 24, 2015  wilayani Kilosa baada ya kutangazwa kwa  matokeo ya uchaguzi wa wabunge wa viti maalumu kwa makundi matano , UWT Mkoa, watu wenye ulemavu, Taasisi za Vyuo Vikuu, Wafanyakazi, NGO’s.

Hivyo aliwaomba  wanawake kuunga mkono juhudi za serikali ya kukabiliana na uharifu wowote kushiriki katika ulinzi shirikishi kwa kutoa taarifa  kwa vyombo vya dola kwa watu wanaoshuku kuwa na  mienendo isiyofahamika  maeneo wanakoishi.

Pia aliomba kamati ya ulinzi na usalama  mitaa, vitongoji , vijiji na kata ziwajibike katika majukumu ya kufanya kazi zao za kubaini waharifu.

Mbali na hayo alitumia fursa hiyo kuwaomba  wananchi wa madhehabu mbalimbali ndani ya mkoa kuwafichua watu wanaogeuza nyumba za ibada kuwa ni sehemu ya maficho yao ya kupanga ama  kutekeleza vitendo vya kiharifu  hali inayoweza kutoa taswira potovu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...