Nabu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Angela Kairuki akizungumza na wanawake katika mkutano wa kuwajengea uwezo wanawake katika masuala ya uongozi uliofanyika katika hoteli ya serena jijini Dar es Salaam.
 Katibu mtendaji wa uongozi institue,Profesa Joseph Semboja  akizungumza katika mkutano wa kuwajengea uwezo wanawake katika masuala ya uongozi uliofanyika katika hoteli ya serena jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wanawake walioshiriki mkutano wa kuwajengea uwezo katika masuala ya uongozi uliofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wanawake walioshiriki mkutano wa kuwajengea uwezo katika masuala ya uongozi uliofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.


NAIBU  Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Angela Kairuki amewataka wanawake kujiamini katika nafasi za uongozi wanazozipata katika kuweza kufikia asilimia ya 50 kwa 50.

Hayo aliyasema katika mkutano wa wanawake ulioandaliwa na uongozi Instute,Kairuki amesema katika kuelekea katika uchaguzi mkuu wanawake wajitokeze katika nafasi mbalimbali ili kuweza kubadilika.

Amesema katika ngazi mbalimbali za maamuzi katika bodi zilizopo nchini ni idadi ndogo za wanawake ikilinganishwa na wanaume hali ambayo sasa inatakiwa kuweka kupaumbele katika bodi kuwa na uwakilishi wa wanawake.

Kairuki amesema sasa ni wakati wa mabadliko kwa wanawake kuonyesha uwezo katika kazi mbalimbali na kujenga mazingira ya kujiamini katika kazi iwe  nafasi za ukurugenzi na kazi nyinginezo za serikali na sekta binafsi.

Nae Katibu Mtendaji wa Uongozi Institute,Profesa Joseph Semboja amesema wameanza program hiyo katika kuwainua wanawake katika nafasi za uongozi katika kuweza kufikia malengo ya asilimia 50 kwa 50.
Sembomja amesema wanawake katika kuelekea uchaguzi mkuu ni fursa kwao kujitokeza kutokana na mafunzo mbalimbali wanayopata kutoka kwa wanawake waliokatika nafazi za uongozi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 01, 2015

    Hata kinamama wanatosha katika nafasi za uongozi. Wanayoyafanya kwa umakini kuhakikisha mambo yanakuwa sawa katika nyumba zao na katika sehemu zao za kazi na biashara, yanawawezesha kuwa na uwezo mkubwa wa kuchukua majukumu zaidi na nafasi mbali mbali za uongozi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...