Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu mafanikio ya wizara yake katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne. Chikawe
alisema kupitia taasisi zake yakiwemo Majeshi ya Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto na
Uokoaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Idara ya Wakimbizi pamoja na Idara zingine
zilizoko chini ya wizara hiyo, imepata mafanikio makubwa hususani katika jukumu la msingi la
ulinzi na usalama wa nchi jambo ambalo limewezesha nchi kuwa na amani na utulivu. Kikao
hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu mafanikio ya wizara yake katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne. Chikawe
alisema kupitia taasisi zake yakiwemo Majeshi ya Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto na
Uokoaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Idara ya Wakimbizi pamoja na Idara zingine
zilizoko chini ya wizara hiyo, imepata mafanikio makubwa hususani katika jukumu la msingi la
ulinzi na usalama wa nchi jambo ambalo limewezesha nchi kuwa na amani na utulivu. Kikao
hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto
ni Mkuu wa Jeshi la Magereza (CGP), John Minja.
Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (D-IGP), Abdulharman Kaniki akijibu swali la mwandishi
wa habari kuhusu uwepo wa vituo vidogo vya polisi nchini (Police Posts) pamoja na majukumu
yake. Kwa mujibu wa D-IGP, vituo hivyo vipo kwa mujibu wa sheria na haviruhusiwi kuwa na
silaha za moto, na endapo askari wa vituo hivyo vidogo wakimkamata mtuhumiwa watampeleka
katika vituo vikubwa vya polisi ili utaratibu mwingine wa kisheria uweze kufanyika. Kiongozi
huyo wa Polisi alipewa nafasi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe ili
kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu vituo hivyo, wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelezea
mafanikio ya wizara katika Serikali ya Awamu ya Nne, uliofanyika katika Ukumbi wa wizara
hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI),
Diwani Athuman. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...