Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kakukuru,Ukerewe ikiwa siku ya mwisho ya ziara yake mkoani Mwanza.
Katibu Mkuu amekamilisha ziara ya kutembelea majimbo yote ya Uchaguzi nchi nzima ambapo amejionea utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi unavyooendelea pamoja na uhai wa Chama Cha Mapinduzi.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Magessa Mulongo akihutubia wakazi wa Kakukuru wilayani Ukerewe.
 Wakazi wa Kakukuru ,Ukerewe wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana kabla ya kuzindua shina la wakereketwa wa CCM Kakukuru.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya maendeleo ya mradi wa maji Kazilankanda uliopo kijiji cha Chabilungo ,Ukerewe utakaonufaisha vijiji 13 kutoka kwa msimamizi wa mradi Revocatus Migarambo .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Nansio katika Uwanja cha Mongella ambapo aliwaambia wananchi hao wasichagueviongozi kishabiki kwani ushabiki unaweza wachelewesha sana kimaendeleo,alitoa mfano halmashauri ya wilaya ya Ukerewe ipo upinzani na hakuna jambo la maendeleo linafanyika mpaka sasa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 01, 2015

    Ukerewe jamani, hata jukwaa la kusimamia badala ya hicho kiti?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...