RAIS wa klabu ya soka ya Simba, Evans Aveva, (pichani juu), jana alikuwa kama kocha wa Chelsea, Josse Morinho, kutokana na jinsi alivyokuwa akiwaelekeza wachezaji wa timu ya viongozi wa Simba dhidi ya timu ya soma ya wasanii wa bongo movie na bongo flava kwenye maadhimisho ya siku ya Simba almaarufu kama Simba Day.
Aveva abaye alikuwa “kaulamba” yaani kapiga suti yake nyeusi, alikuwa ndio “kocha wa timu hiyo ya viongozi wa Simba.
Akiwa amevalia suti nyeusi, hakuweza kutulia kwenye kiti, kila wakati alisimama na kuwaelekeza wachezaji wake kwa kunyoosha mikono na kufoka.
Timu ya soka ya viongozi wa Simba iliibuka mshindi wa bao 1-0.
Baada ya pambano hilo, lilifuatia tendo la kuwatambulisha wachezaji wapya wa Simba na benchi la ufundi kabla ya kuanza kwa pambano maalum la kirafiki baina ya timu hiyo ya mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam na wageni wao Sports Club Villa ya Uganda, katika pambano hilo la kirafikli, Simba iliibanjua Sports Club Villa "Jogoo" bao 1-0. Bao lililofungwa na Awadh Juma, kwenye dakika ya 45 ya kipindi cha lala salama.
Baada ya pambano hilo, lilifuatia tendo la kuwatambulisha wachezaji wapya wa Simba na benchi la ufundi kabla ya kuanza kwa pambano maalum la kirafiki baina ya timu hiyo ya mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam na wageni wao Sports Club Villa ya Uganda, katika pambano hilo la kirafikli, Simba iliibanjua Sports Club Villa "Jogoo" bao 1-0. Bao lililofungwa na Awadh Juma, kwenye dakika ya 45 ya kipindi cha lala salama.
Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Hassan Dalali(kulia)
Kikosi cha timu ya wasanii
Kikosi cha timu ya viongozi wa Simba
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Kikosi cha timu ya wasanii
Kikosi cha timu ya viongozi wa Simba
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...