Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Profesa Idris Kikula akimkabidhi Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi nakala ya kitambu kinachoelezea kwa kina historia ya Chuo Kikuu cha Dodoma.  Katika Maelezo yake,  Prof. Kikula amesema UDOM  imeamua kuweka katika maandishi historia nzima ya  Chuo hili ili kuepusha upotoshaji na upindishaji wa  ukweli na kwamba UDOM  inapanga kumuenzi Mhe. Rais Jakaya Kikwete  ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuanzishwa na hatimaye ujenzi wa UDOM. wengine katika picha kutoka kushoto ni Naibu Mkuu wa Chuo Prof. Shaaban Mlacha anayesimamia masuala ya  mipango, fedha na utawala, Naibu Mwakilishi wa Kudumu Balozi Ramadhan Mwinyi na Bi. Christina Silvester, Katibu wa Baraza.
Makamu Mkuu wa UDOM Prof. Kikula akimkabidhi nakala ya kitambu cha historia ya UDOM,  Prof. Estomih Mtui, M.D  anayefanya kazi  Weill Cornel Medical Collage, Prof. Mtui  ni moja kati ya  wana-Diaspora ambaye  amekuwa  kiungo kikubwa katika utafutaji na upatikanaji wa vifaa tiba ,vitabu na wataalam wa fani mbalimbali kwaajili ya kusaidia nchini Tanzania. baadhi ya  vifaa na vitabu ambavyo  Ujumbe wa   Makamu Mkuu wa UDOM wamevikagua vimepatikana kwa  juhudi za Prof. Mtui

Na Mwandishi Maalum, New York
Chuo Kikuu cha Dodoma ( UDOM), kinatarajia kufanya hafla ya  aina yake ya kumuenzi Rais  wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kama sehemu ya kutambua mchango wake wa hali na mali uliopelekea kuanzishwa kwa Chuo   Kikuu hicho cha aina yake 

Tanzania na nje ya Tanzania.
Taarifa ya kusudio la  Chuo hicho kumuenzi Mh. Rais Kikwete imetolewa mwishoni mwa wiki na Makamu Mkuu wa  UDOM, Prof. Idris Kikula wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na   Mabalozi na Maafisa wa Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika 

Umoja wa Mataifa.Profesa Kikula   na ujumbe wake   yuko  katika ziara ya kikazi nchini Marekani,  ziara iliyomfikisha  Jijini New York, ambapo   ujumbe ulipata fursa ya kukagua vifaa tiba na vitabu  vya kiada na ziada ambavyo vimetolewa na  wadau mbalimbali wenye mapenzi mema na Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...