Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Bi. Fionnuala Gilsenan, akitoa hotuba yake wakati wa maonyesho ya sayansi kwa wanafunzi wa sekondari yanayoandaliwa na shirika la YST ambayo pia Ubalozi wake unadhamini kila mwaka.

Na Daniel Mbega
UBALOZI wa Ireland nchini Tanzania, umewapatia scholarship Watanzania 14 ili kusoma kozi mbalimbali za shahada ya uzamili (masters) na huku wanne kati yao wakienda kusoma vyuo vya nje ya nchi hasa University College Dublin, Dublin Institute of Technology na National University of Ireland Maynooth. 

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ubalozi wa Ireland nchini, scholarship hizo zimetolewa na ubalozi huo kama sehemu ya Mpango wa Mafunzo wa Kila Mwaka (Fellowship Training Programme), ambapo wataalamu wanne waliobahatika kwenda ng’ambo watakwenda kusomea kozi za Maendeleo Endelevu (Sustainable Development), Kilimo na Maisha ya Vijijini (Agriculture and Rural Livelihoods), Rasilimali Watu (Human Resource Management), na Immunolojia na Afya ya Binadamu (Immunology and Human Health).

Watanzania wengine 10 wamedhaminiwa kusomea kozi mbalimbali katika vyuo vikuu vya hapa nchini.Taarifa hiyo inasema, sherehe za kuwapokea wale walihitimu na kuwakabidhi scholarship wale wanaokwenda kuanza, zitafanyika kesho mchana katika ofisi za Ubalozi zilizoko Masaki, jijini Dar es Salaam ambapo Balozi wa Ireland nchini, Fionnuala Gilsenan, ndiye atakayetoa scholarship hizo.

Mpango huo wa Mafunzo wa kila Mwaka, kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwa kiasi kikubwa unahusisha Mfuko wa Misaada wa Ireland (Irish Aid) kupitia program ya maendeleo ya Ubalozi huo nchini Tanzania.
Wanufaika wa mpango huo wameteuliwa na washirika wa maendeleo wa Ireland nchini Tanzania, zikiwemo wizara mbalimbali za Serikali, halmashauri za wilaya na mashirika yasiyo ya kiserikali, ambayo shughuli zao zinawiana na maeneo ya vipaumbele vya Irish Aid, hususan Kilimo, Afya, Lishe na Utawala.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...