Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Bi. Fionnuala Gilsenan, akitoa hotuba yake wakati wa maonyesho ya sayansi kwa wanafunzi wa sekondari yanayoandaliwa na shirika la YST ambayo pia Ubalozi wake unadhamini kila mwaka.
Na Daniel
Mbega
UBALOZI wa
Ireland nchini Tanzania, umewapatia scholarship Watanzania 14 ili kusoma kozi
mbalimbali za shahada ya uzamili (masters) na huku wanne kati yao wakienda kusoma
vyuo vya nje ya nchi hasa University College Dublin, Dublin Institute of
Technology na National University of Ireland Maynooth.
Kwa mujibu
wa taarifa kutoka Ubalozi wa Ireland nchini, scholarship hizo zimetolewa na
ubalozi huo kama sehemu ya Mpango wa Mafunzo wa Kila Mwaka (Fellowship Training
Programme), ambapo wataalamu wanne waliobahatika kwenda ng’ambo watakwenda
kusomea kozi za Maendeleo Endelevu (Sustainable Development), Kilimo na Maisha
ya Vijijini (Agriculture and Rural Livelihoods), Rasilimali Watu (Human
Resource Management), na Immunolojia na Afya ya Binadamu (Immunology and Human
Health).
Watanzania
wengine 10 wamedhaminiwa kusomea kozi mbalimbali katika vyuo vikuu vya hapa
nchini.Taarifa
hiyo inasema, sherehe za kuwapokea wale walihitimu na kuwakabidhi scholarship
wale wanaokwenda kuanza, zitafanyika kesho mchana katika ofisi za Ubalozi zilizoko
Masaki, jijini Dar es Salaam ambapo Balozi wa Ireland nchini, Fionnuala Gilsenan, ndiye atakayetoa scholarship hizo.
Mpango huo
wa Mafunzo wa kila Mwaka, kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwa kiasi kikubwa
unahusisha Mfuko wa Misaada wa Ireland (Irish Aid) kupitia program ya maendeleo
ya Ubalozi huo nchini Tanzania.
Wanufaika wa
mpango huo wameteuliwa na washirika wa maendeleo wa Ireland nchini Tanzania,
zikiwemo wizara mbalimbali za Serikali, halmashauri za wilaya na mashirika
yasiyo ya kiserikali, ambayo shughuli zao zinawiana na maeneo ya vipaumbele vya
Irish Aid, hususan Kilimo, Afya, Lishe na Utawala.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...