Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad akipewa maelezo ya ujenzi wa kituo cha kuwarekebisha watu walioathirika kwa matumizi ya dawa za kulevya huko Kidimni Wilaya ya Kati. Anayetioa maelezo hayo (aliyenyoosha mkono) ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Dk. Omar Dad Shajak. Picha na Salmin Said, OMKR.
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amesifu maendeleo mazuri ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha kuwarekebisha kitabia watu walioingia katika matumizi ya dawa za kulevya kinachojengwa Kidimni Wilaya ya Kati Unguja.
Maalim Seif ameeleza hayo leo wakati alipotembelea ujenzi wa kituo hicho unaofadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambao unakisiwa utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.6 na kujengwa na kampuni ya Alhilal ya hapa Zanzibar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...