Marehemu Mzee SK George Mallya
Familia ya  Mallya inasikitika kutangaza kifo cha Mzee SK George Mallya aliyefariki kwenye hospitali ya KCMC siku ya Jumamosi tarehe 8 Agosti. Taarifa ya familia inaeleza kuwa marehemu  anatarajiwa kuzikwa siku ya Alhamisi tarehe 13 Agosti, nyumbani kwake Maili-Sita, Moshi, ambako mipango ya mazishi inafanywa kwa sasa.
Marehemu Mzee SK George Mallya atakumbukwa kama mmoja wa wanajeshi shupavu wa Kings African Rifles (KAR) wa  Tanganyika Battalion nyakati za Vita Kuu vya Pili (World War Two) ambapo alienda kupigana na Wajapani kule Burma (siku hizi Myanmar).
Baada ya Vita kuisha mwaka wa 1945, alishika nyadhifa mbalimbali katika Serikali za Mitaa, hadi kuwa kiongozi mkuu wa kwanza wa Kiafrika wa Jiji la Dar es Salaam. Baada ya kutoka Serikalini, aliiongoza kampuni ya Lonrho Tanzania hadi alipostaafu na kuhamia Moshi.
Ameacha watoto wanne wa kike na mmoja wa kiume, pamoja na wajukuu na vitukuu kadhaa.

Mungu Ailaze Roho yake 
mahala pema Peponi.

AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. RIP Mzee Mallya mchango wako mkubwa katika nchi hii tumeutambua.

    ReplyDelete
  2. RIP Mzee Mallya

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...