CHAMA CHA DEMOKRASIA NA
MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA
HABARI
KUHUSU MGOMBEA URAIS KUREJESHA
FOMU
Taarifa
inatolewa kwa vyombo vya habari kuwa baada ya hatua ya kuchukua fomu ya kuwania
uteuzi wa ndani ya chama kugombea nafasi ya urais, Mheshimiwa Edward Ngoyai
Lowassa kesho (LEO) Agosti 1, 2015 atarejesha fomu yake kwa ajili ya taratibu zingine
za ndani ya chama.
Shughuli hiyo
itafanyika kuanzia saa 9.00 jioni, ambapo mgombea atakabidhi fomu yake Ofisi ya Katibu Mkuu, Makao Makuu ya
Chama, Kinondoni, jijini Dar es Salaam katika hadhara ikayohudhuriwa na
viongozi wa chama, wanachama, wafuasi, wapenzi na mashabiki wa CHADEMA kutoka
sehemu mbalimbali.
Mheshimiwa
Lowassa atarejesha fomu hiyo akiwa mgombea pekee baada ya kuwa ametimiza
taratibu za kikatiba hususan kupata wadhamini kutoka mikoa mbalimbali nchi
nzima.
Hatua hiyo ya
kurejesha fomu itafuatiwa na taratibu zingine za kikatiba, ikiwa ni pamoja na vikao
vya uteuzi ambavyo vitaketi kwa mujibu wa ratiba ambayo imeshapangwa na chama.
Imetolewa leo Julai 31, 2015 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na
Mawasiliano – CHADEMA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...