Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mh. Edward Lowassa akiwapumbia maelfu ya wafuasi na wapenzi wa vyama vinavyounda UKAWA waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Rwanda Nzovwe, Jijini  Mbeya leo Agosti 14, 2014. Mh. Lowassa na Mgombea mwenza wake Dkt. Juma Haji Duni, walikuwa jijini humo kwa ajili ya zoezi la kutafuta wadhamini wa Tume na kutambulishwa kwa wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mh. Joseph Mbilinyi "Sugu" akimueleza jambo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mh. Edward Lowassa, wakati akiwahutubia wafuasi na wapenzi wa vyama vinavyounda UKAWA waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Rwanda Nzovwe, Jijini  Mbeya leo Agosti 14, 2014.
Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dkt. Juma Haji Duni akiwahutubia maelfu ya wafuasi na wapenzi wa vyama vinavyounda UKAWA waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Rwanda Nzovwe, Jijini  Mbeya leo Agosti 14, 2014.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mh. Freeman Mbowe akipunga mkono pamoja na wafuasi na wapenzi wa vyama vinavyounda UKAWA waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Rwanda Nzovwe, Jijini  Mbeya leo Agosti 14, 2014.

KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Ivi kuna haja ya kupiga kula jamani kwa hali hii???twaweza kutumia fedha za kampeni kwa mambo mengine na kuokoa muda......

    ReplyDelete
  2. Duh.....hahahahaha mie yangu macho, nimejiandaa kutazama watu wanavyotaka kuzuia maji ya mafuriko kwa mkono.....wengine ndio wameshaanza kutoa sheria na matamko ya ajabu ajabu.

    ReplyDelete
  3. Huo Uwanja wa Rwanda umekuwa maarufu sana ktk mikutano ya kisiasa na isiyo ya kisiasa. Kwa nini usijengwe vizuri na kuvutia zaidi? haifai kabisa ulivyo kwa mtazamo wangu. Anyway, hongereni sana kwa nyomi ya watu.

    ReplyDelete
  4. NA BADO HAPO HAJAENDA HUKO AMBAKO CCM IMEBOMOKABOMOKA, YAANI MWANZA,ARUSHA MOSHI. WATAKOMA.
    UNAAMBIWA WATU WAMESHAAMUA, HATA KAMA LIPUMBA AND DR.SLAA WASIMAME NA KUANZA KURUSHA MAWE KWA UKAWA, WATU HAWA HAWATAELEWA KABISA NI KAMA WATAKUWA WANAMPIGIA MBUZI GITAA.

    ReplyDelete
  5. Uwingi wa watu sio kura nyinyi, ingekuwa hivyo kusingekuwapo na haja ya kupiga kura. Tukutane trh 25 oktoba, 2015.

    ReplyDelete
  6. Ankal hii inaongesha umehamia UKAWA rasmi..

    ReplyDelete
  7. Ya Mola mengi. Tukubali tu yaishe maana.

    ReplyDelete
  8. Haijawahi tokea! Never seen before.Twaweza tumia maamuzi ya "wanaounga mkono waseme ndio na wasiounga mkono wasema sio" kuokoa rasilimali nyingi za Taifa.

    ReplyDelete
  9. Ha....hivi huu wingi wa watu ndio kura zitakuwa hivi hivi? Wengi wao wanakwenda kumshangaa Lowassa tu na upendo wake wa madaraka. Ana lipi jipya la kuisema CCM? Kwa kuwa haikumchukulia hatua katika sakata la Richmond? Haya ndio malipo yake.

    ReplyDelete
  10. Zoezi zima la uchaguzi na kanuni zake linatakiwa kwa watanzania wote walioomba nafasi ili wapewe nafasi sawa. Watu wanaweza kuhudhuria mikutano ya vyama vyote vinavyokuja kujinadi karibu yao lakini watachagua wanayemtaka na matokeo ya uchaguzi ndiyo yatakayohesabika mwezi wa kumi kufuatana na taratibu tulizojiwekea kama nchi.

    ReplyDelete
  11. Lowasa na UKAWA ni kama nyerere na TANU..
    nyota ya lowasa yang'ara ..mungu amempa na atapata tuache fitina tutaenda motoni.. aliepewa kapewa. muhimu ni peace & love.. mungu ibariki Tanzania.

    ReplyDelete
  12. Umati wa Mrema au hata Slaa 2010 ilikuwa kama hii na tunaona matokeo yake. Hata kule Kenya Raila mikutano yake ilikuwa na watu wengi sana, lakin siku ya kupiga kura watu wakamchagua Uhuru.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...