Mhe. Jaji Lawrence Gidudu, Rais wa Chama cha
Majaji wa Afrika Mashariki (EAMJA) (wa tatu kushoto) akiendesha Mkutano wa Waheshimiwa
Majaji na Mahakimu wa Jumuiya hiyo, Mkutano huo unahitishwa leo baada ya
wajumbe hao kukubaliana kwa pamoja kuoresha huduma ya utoaji haki kwa umma.
Wengine ni Wajumbe wa Mkutano huo kutoka Tanzania, Kenya na Uganda
Baadhi ya kundi la Washiriki wa Mkutano wakiwa
katika mkutano huo mapema leo, Mkuano huo uanatarajiwa kumalizika leo
Mhe. Robert Makaramba, Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mwanza (wa kwanza kushoto) pamoja na Washiriki
wengine wa Mkutano wakiwa katika Mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu wa
Afrika Mashariki unaoendelea kufanyika katika Ukumbi wa Mkutano wa Malaika
uliopo jijini Mwanza.
Wajumbe wa Mkutano wakiwa nje ya banda la
Mahakama ya Tanzania lililopo katika Hoteli ya Malaika, lengo la kuwepo kwa
banda hilo la Maonesho ni kuwaeleza washiriki wa Mkutano huo juu ya maboresho
mbalimbali yanayoendelea kufanyika ndani ya Mahakama ya Tanzania lenye lengo la
kuboresha huduma ya utoaji haki nchini. Picha na Mahakama.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...