Baada ya kwikwi ya saa takribani 48 wataalamu wa Modewji blog wanakurejeshea hewani Blog yako pendwa.
Watundu wanaovuruga mambo mtandaoni (hackers) walijaribu kuimiliki blog hii kwa kufanya majaribio zaidi ya mara 300 yaliyosababisha mifumo ya kiusalama, kufanyakazi ya ziada kuihami Modewjiblog.
Hata hivyo wataalamu wetu wameziba mianya iliyokuwa imesababisha hali hiyo na sasa tupo pamoja nanyi.
Tunashukuru kwa uvumilivu wenu, tuko pamoja na endelea kuperuzi nasi.
Kwa mawasiliano zaidi tutumie email: info@modewjiblog.com
Imetolewa na Operation Manager, Zainul Mzige.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...