HALMASHAURI ya Wilaya ya Mufindi  Mkoani Iringa ni mingoni mwa  Wilaya saba nchini, zilizochaguliwa na shirika la kimataifa linaloshughulikia mazao ya viazi (CIP) kutekeleza mradi  wa uzalishaji wa viazi lishe vyenye asilimia kubwa ya vitamini “A” ukilinganisha na  aina nyingine ya vyakula kama Mboga, Matunda na Mizizi.

Taarifa iliyotolewa na Afisa ya Habari na Mawasiliano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Bw. Ndimmyake Mwakapiso, imeeleza kuwa, viazi lishe hivyo ni aina ya viazi vitamu vyenye asilimia 90 ya vitamini A vinavyohitajika katika mwili wa binadamu ili kujenga ubongo wa watoto walio chini ya miaka 05, kuimarisha afya ya wajawazito pamoja na uwezo wa kuona kwa kila mwanadamu.  Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi  Mkoani Iringa ni mingoni mwa  Wilaya saba nchini, zilizochaguliwa na shirika la kimataifa linaloshughulikia mazao ya viazi (CIP) kutekeleza mradi  wa uzalishaji wa viazi lishe vyenye asilimia kubwa ya vitamini “A” ukilinganisha na  aina nyingine ya vyakula kama Mboga, Matunda na Mizizi.


Katika kutekeleza adhima hiyo, mradi huo umeanza kutekekelezwa katika vikundi vya wakulima kwa kuotesha mbegu kwenye maeneo yenye miundombinu ya umwagiliaji yaliyopo katika viijiji vya Igomaaa na Lugolofu pamoja bustani zilizopo kwenye vijiji vya Lugema, Mabaoni na Makungu.
 
 Taarifa hiyo imeongeza kuwa mbegu zitakazozalishwa zitagawiwa kwenye vijiji 18 ambayo vimechaguliwa kutekeleza mradi huo kwa kipindi cha miaka mitatu na utekelezaji mara babada ya kwa kipindi cha mvua.

Aidha, endapo Viazi hivyo vitazalishwa kwa wingi na kuongezwa thamani   vitaboresha  kipato kwa mkulima kwani soko lake linapatikana kwa urahisi huku vikiwa na uwezo wa kuzindikwa kwa utengenezaji wa Kripsi, Mkate, Chapati, Biskuti, Juisi na unga wa lishe.  Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi  Mkoani Iringa ni mingoni mwa  Wilaya saba nchini, zilizochaguliwa na shirika la kimataifa linaloshughulikia mazao ya viazi (CIP) kutekeleza mradi  wa uzalishaji wa viazi lishe vyenye asilimia kubwa ya vitamini “A” ukilinganisha na  aina nyingine ya vyakula kama Mboga, Matunda na Mizizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...