Mwamoto akionyesha fomu ya ubunge kulia kwake ni dada wa prof Peter Msolla Anna Msola na kutoka kulia ni msimamizi mkuu wa uchaguzi Rukia Mhango na Msaidizi wake 

Na MatukiodaimaBlog, Kilolo

Mgombea mteule ubunge ccm jimbo la Kilolo Venance Mwamoto ametangaza msahama kwa wajumbe wa kamati ya siasa na wagombea udiwani ambao walikuwa upande wa mbunge wa zamani Prof Peter Msolla huku akiwataka kupenda ili kuwezesha jimbo hilo kupiga hatua ya kimaendeleo  
Mwamoto alisema kuwa hana kinyongo na mgombea yeyeto Kati ya wagombea 15 waliojitokeza na kumwomba prof Msola kuonyesha ushirikiano katika kampeni ili kuwezesha ushindi kwa Mgombea urais wa Ccm Dr John Magufuli ,ubunge na Madiwani wote wa CCM. 
Mwamoto ametoa kauli hiyo Mchana wa leo wakati akitoa kuchukua fomu ya ubunge na kuwawapongeza  wagombea hao wa ccm udiwani kwa kuteuliwa huku akiahidi kuwapa ushirikiano mkubwa katika kata zao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mabango Yake yanakuwa na picha ya diwani kwa kata husika. 
Kwani alisema haipendezi kuona makundi ya kampeni z kura za maoni yanaendelea katika jimbo na kata za jimbo la Kilolo. Hivyo aliwataka wagombea hao wa udiwani kuandika barua za kuwapongeza kwa kushiriki kura za maoni wale wote waliogombea nao pamoja na kuwaomba kushiriki kampeni badala ya kuwabagua na kujigamba kwa kushinda.

Alisema jimbo hilo ili lipige hatua katika maendeleo linahitaji umoja zaidi toka kwa mabalozi, wenyeviti, Madiwani na mbunge

Huku akiwataka Madiwani hao baada ya kushinda kutokwenda katika vikao vya madiwani bila kufanya mikutano na wananchi. 
" Ni marufuku kwa diwani hata Mimi mbunge kwenda bungeni bila ya kuchukua kero za wananchi kwenda bungeni ama katika mabaraza ya Madiwani bila kukutana na wananchi si uwakilishi unaotakiwa " 
Mwamoto alisema kuwa jimbo hilo la Kilolo anataka liwe jimbo la mfano kwa maendeleo katika Mkoa wa Iringa hivyo Kazi Yake kubwa kwa sasa ni kuhakikisha anabainisha changamoto zote na kuanza na chache katika utekelezaji. 
Msimamizi mkuu wa uchaguzi jimbo la Kilolo Lukia Mhango alisema kuwa jumla ya vyama vitatu vimechukua fomu ya ubunge kikiwemo chama cha mapinduzi ,Chausta na ACT wazalendo huku akisema ruksa kwa wagombea kuchukua na kurejesha fomu kwa shamra shamra.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...