Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe
mama Salma Kikwete wakitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza la Kada
Mkongwe wa CCM Marehemu Mzee Peter Kisumo wakati wa ibada ya mazishi
iliyofanyika huko kijijini kwake Usangi- Mwanga Mkoani Kilimanjaro leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji
Mama Hosiana Kisumo Mke wa Marehemu Peter Kisumo wakati wa mazishi yake
huko Usangi Mwanga Mkoani Kilimanjaro.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe
Mama Salma Kikwete wakiweka udongo katika kaburi la Kada Mkongwe wa CCM
Marehemu Peter Kisumo wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwake
Usangi- Mwanga Mkoani Kilimanjaro.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini
kitabu cha maombolezo kilichowekwa kanisani wakati wa mazishi ya kada
mkongwe wa CCM Mzee Peter Kisumo yaliyofanyika kijijini kwake
Usangi-Mwanga Mkoani Kilimnjaro.(Picha na Freddy Maro)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...