TAIFA STARS YAANZA MAZOEZI
KIKOSI
cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kimeanza mazoezi katika uwanja wa
Karume kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria kuwania kufuzu kwa Fainali za
Mataifa ya Afrika mwaka 2017 nchini Gabon.
Wachezaji
wa Taifa Stars chini ya kocha wake mkuu Charles Mkwasa watakua wakijifua mara
mbili kwa siku asubuhi na jioni katika uwanja wa Karume katika kujiweka fit na
maandalizi ya mchezo huo.
Kufuatia
baadhi ya wachezaji kuwa na majukumu na timu zao kujiandaa na mchezo wa Ngao ya
Hisani utakaochezwa Agosti 22, Mkwasa amewaongeza wachezji wengine kumi (10)
kutoka katika orodha yake ya akiba.
Lengo
la kambi hii ya awali ya siku tano, ni kocha mkuu pamoja na benchi lake la
ufundi kupata nafasi ya kuwaona wachezaji katika mazoezi hayo kabla ya safari
ya kuelekea nchini Uturuki Agosti 23 mwaka huu kwa kambi ya siku kumi.
Wachezaji
walioitwa na kuanza mazoezi leo ni Said Mohamed, Vicent Andrew (Mtibwa Sugar),
Mohamed Hussein, Ibrajim Hajibu (Simba SC), Hamis Ali, Juma Mbwana (KMKM),
Tumba Sued (Coastal Unioni), Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Ibrahim Hilka
(Zimamoto– Zanzibar) na Mohamed Yusuf (Prisons).
Wachezaji wengine waliopo kambini ni Said Ndemla, Hassan
Isihaka, Abdi Banda(Simba SC), Rashid Mandawa (Mwadui FC), Michael Aidan (Ruvu
Shooting), Orgeness Mollel (Aspire Academy) na Abdulhaman Mbambi (Mafunzo).
Kwa taarifa zaidi BOFYA HAPA
Kwa taarifa zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...