Kutokana na uhaba wa fedha, Busara Promotions inasikitika kutangaza
kuwa tamasha la Sauti za Busara mwaka 2016 halitakuwepo, hii itakuwa ni
mara ya kwanza ndani ya miaka kumi na tatu Zanzibar kulikosa Tamasha la
kimataifa la Sauti za Busara lifanyikalo kila wiki ya pili ya mwezi
Februari.
Yusuf Mahmoud, Mkurugenzi Mtendaji wa Busara Promotions, amesema leo "Uamuzi huu haukuchukuliwa kwa wepesi”. Kawaida huwa tunatangaza tarehe za tamasha mwaka mmoja kabla. Lakini baada ya kufanya tamasha lililopita kwa mafanikio, tumekuwa katika hali ya ukosefu wa fedha kwa toleo lijalo la 2016.
Yusuf Mahmoud, Mkurugenzi Mtendaji wa Busara Promotions, amesema leo "Uamuzi huu haukuchukuliwa kwa wepesi”. Kawaida huwa tunatangaza tarehe za tamasha mwaka mmoja kabla. Lakini baada ya kufanya tamasha lililopita kwa mafanikio, tumekuwa katika hali ya ukosefu wa fedha kwa toleo lijalo la 2016.
Tulijiwekea malengo ya kukusanya dola za kimarekani
200,000 kabla ya Julai, wakati tulipokuwa na matumaini ya kutangaza
tarehe za Sauti za Busara 2016. Baada ya mikutano mingi na wadau,
tulisogeza muda wetu wa kutafuta fedha hadi usiku wa Agosti 19. Kiasi
ambacho tuna uhakika wa kukipata kuandaa tamasha lijayo kwa sasa
kinasimamia kwenye dola za kimarekani 42,000, hivyo basi bado tuna
safari ndefu mbele yetu.
Kawaida wakati kama huu, tunakuwa tumeshafika
mbali kwenye makubaliano ya mikataba mbalimbali kama ya kukodi ukumbi,
ukodishaji wa vifaa, wasanii na mameneja, tunaanza kupanga ratiba,
maandalizi ya usafiri na malazi kwa wasanii mapema iwezekanavyo.
Shinikizo zaidi, tumekuwa tukipokea maswali kutoka kwa watu mbalimbali
duniani kote wakitaka kujua tarehe za tamasha ili waweze kufanya mipango
yao ya safari. Mauzo ya tiketi za Sauti za Busara haijawahi kuwa
tatizo, lakini hii inasaidia kulipa 30% ya gharama za tamasha ".
Yusuf ameendelea , "Matamasha yanahamasisha vijana kupenda utamaduni wao, hutoa fursa kwa wasanii na wataalamu wa muziki kukutana na kujifunza , yanashawishi uhai wa tamaduni, pia yanatoa nafasi za ajira kwa watu wa ndani na kutoa mifano ya utalii ambayo inathamini na kuheshimu utamaduni wa ndani. Hata hivyo, tangu mwaka 2004 hatuna msaada wowote wa kifedha kutoka serikali ya Zanzibar, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pamoja na jitihada nyingi, msaada kutoka kwa wahisani, balozi na wafanyabiashara unazidi kupungua siku hadi siku. Busara Promotions ni shirika lisilo la kiserikali; tamasha haliko kibiashara.
Yusuf ameendelea , "Matamasha yanahamasisha vijana kupenda utamaduni wao, hutoa fursa kwa wasanii na wataalamu wa muziki kukutana na kujifunza , yanashawishi uhai wa tamaduni, pia yanatoa nafasi za ajira kwa watu wa ndani na kutoa mifano ya utalii ambayo inathamini na kuheshimu utamaduni wa ndani. Hata hivyo, tangu mwaka 2004 hatuna msaada wowote wa kifedha kutoka serikali ya Zanzibar, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pamoja na jitihada nyingi, msaada kutoka kwa wahisani, balozi na wafanyabiashara unazidi kupungua siku hadi siku. Busara Promotions ni shirika lisilo la kiserikali; tamasha haliko kibiashara.
Wengine walipendekeza tujaribu
kuomba pesa kupitia mitandao. Hata hivyo, kwa kweli ili kuwa endelevu
zaidi, kipaumbele chetu kabla ya toleo la 2017 kitakuwa ni kuendeleza
ushirikiano wa muda mrefu na wadhamini na wafadhili ambao wanakubaliana
na mtazamo wetu. Mtu yeyote anaesoma ujumbe huu na ana nia ya kusaidia
kuiweka Sauti za Busara hai, kukuza ajira nchini, wakati tunaendelea
kuung’arisha muziki wetu wenye utajiri wa mila na kukuza utalii wa
kiutamaduni Zanzibar na Tanzania, tafadhali awasiliana nami kupitia
Busara Promotions."
Katika kipindi cha miaka kumi na mbili iliyopita, Busara imewavutia maelfu ya wageni kutoka kila pembe ya dunia kuja Zanzibar , wakati ambayo hakuwa msimu wa wageni wengi . Ndege zote zinazokuja Zanzibar kipindi cha tamasha zinajaa, hoteli na migahawa vinajaa, maduka yaliyopo maeneo ya Mji Mkongwe yanapata wateja wengi zaidi.
Katika kipindi cha miaka kumi na mbili iliyopita, Busara imewavutia maelfu ya wageni kutoka kila pembe ya dunia kuja Zanzibar , wakati ambayo hakuwa msimu wa wageni wengi . Ndege zote zinazokuja Zanzibar kipindi cha tamasha zinajaa, hoteli na migahawa vinajaa, maduka yaliyopo maeneo ya Mji Mkongwe yanapata wateja wengi zaidi.
Hata makadirio
yanaonyesha tangu mwaka 2004 tamasha limekiingizia kisiwa mapato ya
kiasi dola za kimarekami milioni 70. Wakati huo huo, Shirika la
utangazaji la BBC limeiweka Sauti za Busara kama moja ya "matamasha ya
muziki bora na ya kuheshimika zaidi Afrika ". Pia limeingizwa kwenye
CNN "matamasha 7 ya muziki ya kiAfrika unayotakiwa kuyaona" na kileleni
kwenye orodha ya AfroTourism ya "Matamasha bora ya Muziki ”
Yusuf Mahmoud hatimaye alisema " Wakati mwingine ni muhimu kupiga hatua moja nyuma, kabla ya kusonga mbele. Bodi na uongozi wa Busara itafanya kazi kwa bidii zaidi miezi ijayo, ili kuhakikisha kuanzia mwaka 2017 tamasha linarudi kuwa na nguvu zaid
Yusuf Mahmoud hatimaye alisema " Wakati mwingine ni muhimu kupiga hatua moja nyuma, kabla ya kusonga mbele. Bodi na uongozi wa Busara itafanya kazi kwa bidii zaidi miezi ijayo, ili kuhakikisha kuanzia mwaka 2017 tamasha linarudi kuwa na nguvu zaid
i. Inawezekana itamaanisha kuhama
eneo, au kulifanya kila baada ya miaka miwili . Hakika vipaumbele vyetu
vitakuwa kulifanya tamasha litoe nafasi zaidi kwa wananchi , wakati
tunaelendea kuomba kujenga ushirikiano wa muda mrefu , na sekta za umma
na binafsi".
Wakati tamasha likiwa kwenye mapumziko, Busara Promotions itaendelea na shughuli zake za kawaida za kukuza muziki wa kiAfrika, kuimarisha uelewa wa watu na kuboresha sekta ya muziki. Kwa mwaka mzima, Busara itahakikisha wasanii wa Afrika Mashariki wanapata mialiko kwenye matamasha mengine ya kimataifa na kuwezesha kujenga ujuzi kwa wasanii wa ndani na wafanyakazi wa tamasha, kwa njia ya kubadilishana na mafunzo ya uongozi wa sanaa, masoko, habari na ujuzi wa kiufundi . Kazi hii , ambayo inadhaniniwa na Ubalozi wa Norway , Dar es Salaam , haitotetereshwa na uamuzi wa kufuta Sauti za Busara 2016 .
Wakati tamasha likiwa kwenye mapumziko, Busara Promotions itaendelea na shughuli zake za kawaida za kukuza muziki wa kiAfrika, kuimarisha uelewa wa watu na kuboresha sekta ya muziki. Kwa mwaka mzima, Busara itahakikisha wasanii wa Afrika Mashariki wanapata mialiko kwenye matamasha mengine ya kimataifa na kuwezesha kujenga ujuzi kwa wasanii wa ndani na wafanyakazi wa tamasha, kwa njia ya kubadilishana na mafunzo ya uongozi wa sanaa, masoko, habari na ujuzi wa kiufundi . Kazi hii , ambayo inadhaniniwa na Ubalozi wa Norway , Dar es Salaam , haitotetereshwa na uamuzi wa kufuta Sauti za Busara 2016 .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...