Mwenyekiti wa Jumuiya  ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Tanzania (TSSA),Eliud Sanga  ( kati kati) ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa(LAPF), akibadilishana mawanzo na  Katibu mkuu wa  TSSA, Meshack Bandawe, ( kulia) ambaye pia ni Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa ,  Augosti 24, mwaka huu mjini Morogoro  baada ya mwenyekiti huyo kufungua mafunzo kwa wafanyakazi wa mbalimbali wa mifuko yote ya hifadhi ya jamii chini inayounda  Jumuiya hiyo ( kushoto) ni Ofisa Matekelezo wa Mfuko wa PSPF Makao makuu Dar es Salaam.

Na John Nditi, Morogoro
JUMUIYA ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Tanzania (TSSA) umewataka vijana wanaoajiriwa katika mifuko inayounda jumuiya hiyo kuingiza mawazo mapya ya ubunifu  katika  kubuni mbinu mbadala za vivutio ili kukubalika katika soko  katika maeneo ya vijijini ambako huduma hizo  hazijawafikia watu wengi.

 Hayo yalisemwa na Mwenyekiti  wa TSSA,  Eliud Sanga , Augosti 24,mwaka huu , wakati alipofungua mafunzo ya siku tano kwa wafanyakazi mbalimbali wa kutoka mifuko yote ya hifadhi ya jamii chini inayounda  Jumuiya hiyo . 

 Alisema kuwa,  soko bado ni kubwa la kutatafuta wanachama walio nje ya ajira isiyorasmi kuwaingiza katika mifuko hiyo hivyo ni vyema  wakaanza kuelekeza nguvu zao katika kutafuta wanachama  maeneo ya vijijini ambako kuna idadi kubwa ya wananchi wanaohitaji huduma zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...