
Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw.HAB Mkwizu akifungua mkutano wa
kwanza wa mwaka wa Serikali Mtandao leo jijini Arusha.Zaidi ya wataalam
wa TEHAMA 500 kutoka Wizara, Idara, Wakala,Taasisi, Halmashauri wako
jijini Arusha kujadili mafanikio na changamoto za Serikali mtandao.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya
Serikali Mtandao Dkt.Jabiri Bakari akitoa ufafanuzi kuhusu Serikali
Mtandao kwa washiriki wa Mkutano wa kwanza wa Serikali Mtandao
unaofanyika katika ukumbi wa AICC jijini Arusha leo.

Mtaalam wa masuala ya Serikali
Mtandao kutoka nchini Singapore Bw.Tan Kim akiwasilisha mada kuhusu
Umuhimu wa Serikali mtandao kwa washiriki wa Mkutano wa kwanza wa
Serikali mtandao unaofanyika jijini Arusha leo


Wataalam wa Teknolojia ya Habari
na Mawasiliano kutoka maeneo mbalimbali nchini wakifuatilia Masuala
mbalimbali wakati wa mkutano wa kwanza wa mwaka wa Serikali mtandao
unaofanyika jijini Dar es salaam.
Picha na Aron Msigwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...