Katibu Mkuu Ofisi
ya Makamu wa Rais Sazi Salula akifungua Mkutano wa wadau wa mazingira unaohusu
Miradi ya majaribio nchini wa Mkakati wa Kupunguza Uharibifu wa Misitu
(MKUHUMI) leo jijini Dar es salaam.
Kiongozi wa wawezeshaji
kutoka Asasi isiyo ya kiserikali ya Niras kutoka Finland inayosimamia Miradi ya
majaribio nchini wa Mkakati wa Kupunguza Uharibifu wa Misitu (MKUHUMI) Merja
Makela akitoa mada wakati wa mkutano wa wadau wa mazingira kuhusu namna bora ya
kuhifadhi mazingira na kuboresha usimamizi wa ardhi na kuongeza mapato kutoka
kwenye misitu. Mkutano huo ambao umefanyika leo jijini Dar es salaam
umeandaliwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Norway.
Katibu Mkuu Ofisi
ya Makamu wa Rais Sazi Salula (kushoto) akifuatilia mada wakati wa mkutano wa
wadau wa mazingira kuhusu namna bora ya kuhifadhi mazingira na kuboresha
usimamizi wa ardhi na kuongeza mapato kutoka kwenye misitu. Wa pili kushoto ni
Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Julius Ningu.
Picha na Eleuteri
Mangi-MAELEZO).
Na Jenikisa
Ndile-MAELEZO
Watanzania wameaswa
kuzingatia namna bora ya kuhifadhi mazingira, upangaji wa matumizi bora ya
ardhi na utekelezaji wa mipango ili kuleta tija na maendeleo endelevu nchini.
Kauli hiyo imetolewa na
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Sazi Salula leo jijini Dar es salaam
alipokuwa akifungua Mkutano wa wadau wa mazingira unaohusu utekelezaji wa
miradi ya majaribio ya Mkakati wa Kupunguza Uharibifu wa Misitu (MKUHUMI)
nchini.
Bw. Sazi alisema kuwa
mipango hiyo ya MKUHUMI inalengo la kuondoa umasikini kwa watanzania waishio
vijijini ambao wapo karibu na hifadhi za misitu
inasimamiwa na kutekelezwa kwa kushirikiana na Serikari ya kijiji ili
kuhakikisha mafanikio yanapatikana kwa kuzingatia utekelezaji na usimamizi wa
sheria kupitia kamati za vijiji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...