Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na Baltiki, Mhe. Dora Msechu amewasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Rais wa Iceland, Mhe. Ólaf Ragnar Grimsson 
 Mhe. Balozi Dora Msechu sasa amekamilisha kazi ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwenye nchi zote nane za Eneo lake la Uwakilishi; Sweden, Denmark, Estonia, Finland, Iceland, Latvia, Lithuania na Norway. 
 Mhe. Balozi Dora Msechu amepata pia fursa ya kutembelea Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa, tawi la Iceland na kukutana na Mkuu wa Chuo Bw. Ludvik Georgsson kwa madhumuni ya kuwatafutia Watanzania fursa za masomo chuoni hapo kwenye fani ya joto ardhi (Geothermal).
Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na Baltiki, Mhe. Dora Msechu akiwa na na Rais wa Iceland (HOM Iceland) pamoja na Bw. Yusuph Mndolwa, Afisa Ubalozi, baada ya kuwasilisha hati za utambulisho leo

Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na Baltiki, Mhe. Dora Msechu akiwa na na Rais wa Iceland (HOM Iceland) baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na Baltiki, Mhe. Dora Msechu akiwa katika mazungumzo  na Rais wa Iceland (HOM Iceland)  baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na Baltiki, Mhe. Dora Msechu akilakiwa na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa, tawi la Iceland Bw. Ludvik Georgsson. Katikati  ni Bw. Ngereja Mgejwa, Mwanafunzi wa Kitanzania anayesoma Chuoni hapo.
Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na Baltiki, Mhe. Dora Msechu katika mazungumzo ya kuombea watanzania nafasi za masomo na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa, tawi la Iceland Bw. Ludvik Georgsson. Katikati  ni Bw. Ngereja Mgejwa, Mwanafunzi wa Kitanzania anayesoma Chuoni hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...