Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
BENKI ya DCB imekutanisha viongozi wa  mifuko ya kuweka na Kukopa (SACCOS) kuweza kuwapa fursa mbalimbali zilizopo katika benki hiyo.
Akizungumza na viongozi wa SACCOS,Meneja Mwandamizi wa Biashara Ndogo na Kubwa,Haika Machaku,amesema benki ya DCB iko karibu na SACCOS katika kupata fursa za utuzaji wa Amaana na huduma mbalimbali kwa gharama  nafuu.

Amesema wataendelea kushirikiana  na SACCOs kuangalia watavyoweza kusaidiana katika kuimarisha saccos pamoja na wanachama kunufaika na mikopo katika benki hiyo.

Aidha amesema kuwa  nia ya benki kuahakikisha wanachama wananufaika na benki  katika kuendeleza maisha kupitia fursa ambazo benki imeanisha kuinua wajasiriamali  pamoja na ushirika ikiwemo SACCOS.

Benki imewataka viongozi wa SACCOs  kufungua akaunti katika benki hiyo katika kuweza kuanza kufanya kazi  kwa ushirikiano na fursa zao ziweze kuwafikia wanachama.
 Meneja wa Mwandamizi wa Biashara Ndogo na Kubwa wa Benki ya DCB,Machaku,akizungumza na viongozi mbalimbali wa Saccos juu  ya fursa zinazopatikana katika benki ya DCB leo Makao Makuu ya DCB jijini Dar es Salaam.
 Meneja Masoko wa Benki ya DCB, Boyd Mwaisame akizungumza na viongozi wa SACCCOs  jinsi watavyoshirikiana katika kuinua SACCOs,leo Makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa SACCOS ya Wafanyakazi wa TRL,Gwammy Mwakangale Akichangia maada katika mkutano wa DCB  juu ya faida zinaziopatikana katika benki hususani mikopo ya nyumba leo Makao Makuu ya DCB,jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki  ya viongozi wa SACCOs wakiwa katika mkutano ulioitishwa na benki ya DCB kuwapa fursa zinazopatikana katika benki hiyo leo jijini Dar es Salaam.
picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...