Kikosi kazi cha Timu ya Mbeya City fc kikiongwozwa na Gorikipa
mahiri Juma Kaseja katika picha waki mwomba Mwenyezi munu kabla ya kuanza Mtanange, ambapo
Kagera Sugar iliibuka mshindi kwa kuitundika Mbeya City fc Gori Moja
kwa bila (1,0) Dakika ya 41, Mchezaji Poul Ngaiyoma Jezi Nambari 8,
Mgongoni kuipatia ushindi Timu ya Kagera Sugar katika Mechi ya Kwanza
Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara Mtanange ulio chezwa katika Uwanja
wa Sokoine Jijini Mbeya.
Juma
Kaseja Jezi Nambari Moja Mgongoni akiwa makini Lango la Mbeya City
katika Mtanange wa Mbeya City fc na Kagera Sugar, ambapo Kagera Sugar
iliibuka kidedea kwa Gori moja kwa Sifuli (1,0).
Mashabiki wa Mbeya City fc wakishangilia katika Mtanange
uliopigwa katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya ligi kuu ya Vodacom
Tanzania Bara, Kagera moja huku Mbeya City fc Mama kajabwela Tumbo
kamsokota Tumbaku Bilaaa..
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...