KWAYA tatu za muziki wa Injili Tanzania zinatarajia kuwa mojawapo ya wadau watakaoiombea amani Tanzania kuelekea uchaguzi Mkuu kupitia Tamasha la Amani linalotarajia kufanyika Oktoba 4.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama pamoja na kwaya hizo maombi hayo ya amani yatashirikisha waimbaji wengine wa Tanzania na nje.
Msama alizitaja kwaya hizo ni pamoja na Kwaya ya Uinjilisti ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam, Kwaya ya Mtakatifu Andrew Anglican ya Dodoma sambamba na kwaya ya Wakorintho wa pili ya Mafinga mkoani Njombe.

Msama alisema Watanzania wajiandae kupata neno la Mungu lenye lengo la kuombea amani nchi yao kupitia viongozi wa dini na wadau wengine.
"Suala la amani linatakiwa kuzungumzwa na kila mmoja, hivyo ni wakati wa kuunganisha nguvu pamoja kwa lengo hilo," alisema Msama.

Msama alisema kamati yake inaendelea na mchakato wa kufanikisha tamasha hilo ambalo litaunganisha nguvu kumfikia Mungu kwa maombi.

Aidha Msama alisema baada ya kumalizika kwa tamasha hilo jijini Dar es Salaam, Oktoba 6 tamasha hilo litafanyika Morogoro, Oktoba 8 (Iringa), Oktoba 10 (Makambako), Oktoba 11 (Mbeya), Oktoba 13 (Dodoma), Oktoba 14 (Singida), Oktoba 15 (Tabora), Oktoba 16 (Shinyanga) na Oktoba 18 (Mwanza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...