WATU wengi wanafikiri mafanikio ni kitu ambacho kinatokea tuu kama ajali lakini mafanikio sio ajali wala sio bahati mafanikio ni mipango dhahiri ambayo inapangwa na mtu anayeyataka na ayenuia kutoka katika vilindi vya moyoni mwake kwamba anataka kutoka katika sehemu moja kwenye maisha ambayo inakuwa ni duni na kwenda sehemu nyingine ambayo ni ya hadhi nzuri.

Wengi wamekuwa wakijidanganya kwamba ipo siku moja watafanikiwa (watatoboa)lakini hawana mpango wowote wa kuwawezesha kufanikiwa katika iyo siku moja na nataka niwaambie kwamba iyo siku moja haitakaa itokee kama hauna mpango dhahiri wa kupata unachokitaka katika maisha yako.

Unatakiwa kuwa na picha halisi ya kitu unachokitaka kwanza ndipo uende ukakitafute, kumbuka kumiliki kunaanzia kwenye akili kwanza acha kusema nahitaji nyumba nzuri,gari zuri,biashara nzuri, wakati hujapata picha halisi katika akili yako kile unachokihitaji unataka kiweje. Vijana wengi wamekuwa wakimaliza chuo Kikuu na kusema nipo tayari kufanya chochote huu ni ujinga na kutokuwa na maono hivi kweli kama upo tayari kufanya chochote nkikuambia ukachimbe vyoo utachimba? Be definate (unataka nini kwanza) na hicho unachokitaka hakikisha una picha yake kwenye akili yako jinsi kitakavyokuwa ndipo unaanza jitihada zote zitakazokupelekea kupata kile unachohitaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...