Meneja Ufanisi wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, BGML, unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia, Elias Kasikila, (kushoto), akiagana na baadhi ya vijana wanaokwenda kuhudhuria mafunzo ya ufundi chini ya mpango wa IMTT unafadhiliwa na mgodi huo, wakati wa hafla ya kuwaaga iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye eneo la mgodi, huko Msalala mmoani Shinyanga. Mgodi huo umetuamia kiasi cha zaidi ya  nusu bilioni kila mwaka kufadhili mpango huo

Na K-VIS MEDIA
MGODI wa dhahabu wa Bulyanhulu, BGML, unaomilikiwa na kampuni ya uchimbaji na utafutaji madini ya Acacia, umetumia kiasi cha zaidi ya shilingi nusu bilioni kila mwaka, kufadhili mafunzo ya ufundi kwa vijana, chini ya mpango wa IMTT.

Mpango wa kufadhili mafunzo ya IMTT, (Integrated Mining Technical Training), ulianzishwa mnamo mwaka 2009, ambapo mgodi huo hutoa fedha kufadhili elimu hiyo kwa vijana wenye elimu ya kidato cha nne ambao walisoma kwenye shule zilizoko vijiji 14 vinavyozunguka mgodi huo na kushindwa kuendelea na kidato cha sita kwa sababu mbalimbali lakini wawe na umri usioozidi miaka 25.

Akizungumza kwenye hafla ya kuwaaga vijana 20 kutoka vijiji hivyo kwenye mgodi huo, mwishoni mwa wiki ambao wameenda kuanza mafunzo hayo yanayochukua muda wa miaka kati ya mitatu na miwili kwenye chuo cha VETA-Moshi, Menenja Ufanisi (OE),wa BGML, Elias Kasikila, alisema, ufadhili huo ni utekelezaji wa sera ya mgodi kushirikiana na wenyeji wao, (wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka mgodi), katika kujenga mahusiano mema.

Akielezea utaratibu wa kuwapata vijana hao, Kasikila alisema, waombaji hupeleka maombi yao kwenye ofisi za serikali za vijijina kisha maombi hayo kukabidhiwa kwa uongozi wa mgodi ambao huyaachuja kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.

“Sharti muombaji awe amefaulu masomo ya Kiingereza na Hisabati, lakini kupitia kitengo chetu cha usalama, vijana hao huchunguzwa tabia zao huko walikotoka, ikiwa ni pamoja na kufanyiwa vipimo vya kiafya na wanaokidhi vigezo hivyo huchaguliwa.” Alifafanua
Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na ufundi umeme kwa miaka mitatu, fitting na uchomeleaji vyuma, kwa miaka miwili, Diesel mechanic and Instrument, kwa miaka mitatu.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...