Rais wa Baraza Kuu la 69 la Umoja wa Mataifa, Bw. Sam Kutesa akigonga nyundo maalum kuashiria kukamilika kwa Mikutano ya Baraza hilo ambalo ameliongoza kwa mwaka  mzima. Kushoto kwake  ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon akiwa mwenye furaha wakati wa kuhitimishwa  Baraza la 69 ambapo alimpongeza Bw. Sam Kutesa kwa kuliongoza  Baraza kwa uhodari  uliopelekea kupitishwa kwa maazimio mbalimbali.
Na Mwandishi Maaalum New York
Mkutano wa  69 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  uliokuwa chini ya urais wa  Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Bw, Sam Kutesa   umefikia ukingoni siku ya jumatatu  kwa kupitisha maamuzi  ya kihistoria ambayo pamoja na mambo mengine yanatoa mwelekeo wa majadiliano kuhusu marekebisho na mageuzi ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Maamuzi hayo ambayo kwa mara ya kwanza yanaingizwa rasmi katika nyaraka muhimu za  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  na yaliyopewa namba A/69/L.92 yalipitishwa kwa kauli moja  na wajumbe  kutoka nchi 193 wanaounda  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Maamuzi hayo ambayo baadhi ya wazungumzaji waliyapachika  jina kama maamuzi ya Kutessa ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika kusimamia kidete   majadiliano kuhusu mageuzi ya  Baraza Kuu la Usalama la Umoja  wa Mataifa  yanatoa msingi  au maandishi  ambayo kwayo   yatawawezesha nchi wanachama kujadiliana kwa  kupitia maamuzi hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...