(i)
Kutozingatia
muda wa kumaliza Mikutano ya Kampeni
Kuna baadhi ya Vyama ambavyo katika mikutano yao
vimekiuka Kipengele hiki kwa kufanya mikutano zaidi ya saa 12.00 jioni. Kuendelea kufanya Mkutano wa Kampeni zaidi ya
muda huo ni ukiukwaji wa Kipengele cha
2.1 (c) cha Maadili ya Uchaguzi wa
Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015 kinafafanua kuwa Mikutano yote ya Kampeni
itafanyika kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
(ii)
Kubandika
mabango ya Kampeni, matangazo au Mchoro wowote kwenye maeneo yasiyoruhusiwa au
bila idhini ya wahusika
Baadhi ya Vyama vimeanza kubandika mabango, michoro
na picha za Wagombea wao katika majengo au vyombo vya usafiri vya watu binafsi
au Taasisi mbalimbali bila idhini ya wamiliki husika.
Napenda kuwakumbusha kuwa, kwa mujibu wa Kipengele cha 2.2. (g) cha Maadili ya
Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015, hairuhusiwi kufanya hayo
bila idhini ya wamiliki husika.
(iii) Kuchafua, kubandua au kuharibu
matangazo au picha za Kampeni za Vyama vingine
Tume imeanza kupokea malalamiko kutoka baadhi ya
Vyama kuwa, mabango au picha za Kampeni za Vyama vyao yanabanduliwa au
kuchafuliwa na wafuasi wa Vyama vingine.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...