Kipa wa timu ya soka ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akichupa kuzuia mpira wa penati bila mafanikio wakati timu hiyo ilipomenyana na ile ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, NHIF, wakati wa bonanza la pamoja la taasisi hizo mbili lililoandaliwa na PPF na kufanyika kwenye viwanja vya Chuo Cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama jijini Dar es Salaam leo Septemba 5, 2015. Katika bonanza hilo ambalo mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi wa Uwekezaji wa PPF, Steven Alfred, akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu, zawadi mbalimbali zilitolewa kwa washindi wa michezo ya kuvuta kamba, kukimbiza kuku, mbio za magunia, soka na mpira wa wavu. (Volleyball)

NA K-VIS MEDIA
MFUKO wa Pensheni wa PPF, na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, NHIF, wamefanya bonanza la michezo kwenye uwanja wa Chuo Cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama jijini Dar es Salaam, leo Septemba 5, 2015 ili kuonyesha ushirikiano.



Akizungumza kwenye bonanza hilo, mgeni rasmi ambaye alikuwa ni Mkurugenzi wa Uwekezaji wa PPF, akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, amesema, bonanza hilo limewakutanisha pamoja wafanyakazi wa taasisi hizo mbili za umma, ili kuonyesha mshikamano na ushirikiano sio tu katika Nyanja ya kazi bali pia katika Nyanja ya michezo na burudani.
Bonanza hilo lilishirikisha michezo ya kuvuta kamba, soka, mpira wa wafu (Volleyball), mbio za magunia, na kufukuza kuku, ambapo washindi walijinyakulia zawadi mbalimbali. (Picha zote na K-VIS MEDIA/Khalfan Said)

 Mazoezi ya viongo kwa wote
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...