Ofisa Madini Mkazi wa Kahama, Bibi Sophia Omar, akifungua mafunzo kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini kuhusu matumizi ya huduma mpya ya utoaji wa leseni za madini kwa njia ya mtandao. Mafunzo hayo yamefanyika leo Septemba 11, 2015 mjini Kahama ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa na Wizara ya Nishati na Madini kwa wachimbaji wadogo nchi nzima.

Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni cha Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Nuru Shabani, akiwasilisha mada kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni wilayani Kahama, kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao. Semina hiyo imefanyika Septemba 11, 2015 mjini Kahama ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa na Wizara husika kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini kote.

Na Veronica Simba - Kahama
Serikali imesema wachimbaji wadogo wa madini wanaruhusiwa kumiliki idadi yoyote ya leseni za madini ilimradi waweze kuzifanyia kazi.

Hayo yamesemwa leo Septemba 11, 2015 mjini Kahama na Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni, Mhandisi Nuru Shabani wakati akiwasilisha mada kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao, wakati wa semina iliyofanyika mjini humo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...