Mtalaam wa masuala ya Biogesi na Majiko Sanifu wa Taasisi ya kuendeleza Nishati Asilia na Uhifadhi wa Mazingira Tanzania ( TaTEDO) Bw.Stephen Boniface akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu ujenzi wa mtambo wenye uwezo wa kuzalisha gesi yenye mita za ujazo 200 walioujenga katika shule  ya Sekondari Manzese iliyoko wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam jana. Kulia kwake ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Manzese Bw.Linus Mwakasege.
 Mkuu wa Shule ya Sekondari Manzese Bw.Linus Mwakasege akitoa ufafanusi kwa waandishi wa habari kuhusu manufaa ya mradi wa nishati endelevu ya Biogesi utakavyowanufaisha wanafunzi wa shule hiyo.
 Mtaalam wa Nishati Endelevu na mabadiko ya Tabia nchi Bw. Shima Sango kutoka Taasisi ya Uendelezaji wa Nishati asilia na Uhifadhi wa Mazingira (TaTEDO) Akiwasha moja ya jiko la gesi liliojengwa katika shule ya Sekondari Manzese.
Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.
 
 
Na.Aron Msigwa-MAELEZO
SHULE za Sekondari kote nchini zimeshauriwa kuwekeza katika matumizi ya Nishati endelevu ya Biogesi na majiko sanifu ili kulinda na kuhifadhi mazingira.

Ushauri huo umetolewa na Meneja Uhusiano wa Jamii wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam  (DAWASA) Bi.Neli Msuya mara baada ya kutembelea ujenzi wa Mradi wa kuzalisha Nishati endelevu ya Biogesi katika Shule ya Sekondari Manzese wilayani Kinondoni, jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam ( DAWASA ) ikishirikiana na Taasisi ya Kuendeleza Nishati Asilia na Uhifadhi wa Mazingira (TaTEDO)na  Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa UN- HABITAT wameamua kuitumia changamoto  ya uhifadhi wa Maji Taka iliyokuwa inaikabiri shule hiyo kwa kuanzisha mradi wa kuyageuza maji taka ya vyoo vya shule hiyo kuwa rasilimali ya kuzalisha nishati endelevu ya Biogesi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...