Na Ally Daud –MAELEZO
Idadi ya mauzo katika soko la hisa la Dar es salaam DSE limeshuka kwa asilimia 62 kutoka shilingi bilioni 6.4 hadi kufikia shilingi bilioni 2.4 ambapo zimeuzwa na kununuliwa katika soko zimeshuka kutoka milioni 4.3 hadi kufikia milioni 2.7.

Akiongea na waandishi wa habari Meneja Miradi na Biashara waDar es salaam Stock Exchange  Bw. Patrick  Mususa alisema kuwa hata hvyo idadi ya mtaji katika soko umekuwa kutoka tilioni 21.9 hadi tilioni 22.3 ikiwa pia na idadi ya mtaji wa makampuni ya ndani imekua tilioni 9.9.

AidhaBw. Mususa ameitaja benki ya CRDB kuwa ndiyo imeongoza kwa kuuza hisa zake katika soko ikiwa na asilimia 92 ziki fuatiwa na Kampuni ya Swissport yenye asilimia 4 na Twiga Cement ambayo ina asilimia 1.

“Kampuni ambazo zimeongoza kwa ongezeko la bei katika soko la hisa ni Kenya Airways yenye asilimia 9 pamoja na Kampuni ya bia ya East Africa Breweries ambayo ina asilimia 6 pamoja na Kampuni ya uchimbaji wa madini ya Acacia yenye asilimia 3”,alisema Bw.Mususa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...