Na Ally Daud –MAELEZO
Idadi ya mauzo katika soko
la hisa la Dar es salaam DSE limeshuka kwa asilimia 62 kutoka shilingi bilioni 6.4
hadi kufikia shilingi bilioni 2.4 ambapo zimeuzwa na kununuliwa katika soko zimeshuka
kutoka milioni 4.3 hadi kufikia milioni 2.7.
Akiongea na waandishi wa
habari Meneja Miradi na Biashara waDar es salaam Stock Exchange Bw. Patrick Mususa alisema kuwa hata hvyo idadi ya mtaji katika
soko umekuwa kutoka tilioni 21.9 hadi tilioni 22.3 ikiwa pia na idadi ya mtaji wa
makampuni ya ndani imekua tilioni 9.9.
AidhaBw. Mususa ameitaja
benki ya CRDB kuwa ndiyo imeongoza kwa kuuza hisa zake katika soko ikiwa na asilimia
92 ziki fuatiwa na Kampuni ya Swissport yenye asilimia 4 na Twiga Cement ambayo
ina asilimia 1.
“Kampuni ambazo zimeongoza
kwa ongezeko la bei katika soko la hisa ni Kenya Airways yenye asilimia 9 pamoja
na Kampuni ya bia ya East Africa Breweries ambayo ina asilimia 6 pamoja na Kampuni
ya uchimbaji wa madini ya Acacia yenye asilimia 3”,alisema Bw.Mususa.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...