DAR ES SALAAM, Tanzania. Tarehe 21 Septemba 2015 -- Symbion Power yenye tawi lake maeneo ya Ubungo leo imetangaza kuwa imefanikiwa katika majaribio ya kutumia gesi asilia katika mitambo yake . Gesi inapatikana  Ghuba ya  Mnazi iliyo karibu na Mtwara Kusini mwa Tanzania. 

Kwa zaidi ya Mwaka mmoja sasa ; Mitambo hii yenye uwezo wa kuzalisha kiasi cha Megawati 120 haikuweza kufanya uzalishaji wowote kutokana na ukosefu wa gesi asilia kama chanzo cha nishati Tanzania

“Kwa mara nyingine Symbion ina uwezo wa kufanya kazi kwa kutumia gesi asilia badala ya kutumia nishati ya mafuta ambayo pamoja kuwa ni aghali Symbion ililizamika kuitumia kati ya mwaka 2012 na 2014” alinena Mtendaji Mkuu Bwana Paul Hinks. 
Kwa hivi sasa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) nalo litaweza kuendesha mitambo yake kadhaa ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi kutoka Mtwara. 
Aidha Bwana Hinks aliongeza na kusema “ Hii ni habari njema kwa TANESCO ambayo imekuwa na wakati mgumu kifedha kutokana na gharama kubwa inayotumia kununulia mafuta ambayo huingizwa kutoka nchi za nje. Matokeo ya utumiaji gesi asilia katika kuzalisha umeme yatapelekea kuwepo kwa matokeo chanya kifedha kama matokeo mtambuka ya gharama nafuu za uzalishaji umeme”. 
Mitambo ya Symbion Power iliyoko maeneo ya Ubungo ilikuwa ni eneo kuu ambalo Rais Barack Obama alilitumia kuhutubia mnamo Julai mwaka 2013 ambapo pamoja na mambo mengine aliainisha dhana yake ya “Power Africa” ambayo yaweza kutafsiriwa kama Afrika yenye Umeme.Hii dhana ililenga kwenye kuongeza upatikanaji wa umeme mara mbili katika nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara. Kama sehemu ya “Afrika yenye Umeme” Symbion imedhamiria kuwekeza kiasi cha dola za kimarekani billion 1.8 katika sekta ya Umeme kwenye nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara kati ya Julai 2013 mpaka Julai 2018. 
 Kampuni ya Symbion kwa kushirikiana na TANESCO; ziko katika harakati ya kutengeneza mitambo mingine yenye uwezo wa kuzalisha kiwango cha Megawati 600 huko Mtwara. Pamoja na hilo kutakuwepo nguzo za kusambaza umeme mpaka Songea Magharibi huko Kusini mwa Tanzania na kusini mwa Msumbiji. Mara hii miradi itakapokamilika; itaifanya Mtwara kuwa kitivo kikuu cha nishati; kwa maana hiyo itasaidia kuleta umeme ambao unahitajika sana kwenye eneo hilo na hivi kusaidia katika kutengeneza maelfu ya ajira nchini Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...