Katika ukurasa wa mbele na wa tano wa Gazeti la Nipashe, toleo 0578604 la tarehe 12 Septemba, 2015 kumechapishwa taarifa kwamba “Sefue; Marufuku kutumia magari ya serikali kwenye kampeni”

Katika taarifa hiyo, imeelezwa kwamba Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema “Ni kosa kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutumia rasilimali za serikali yakiwemo magari katika mikutano ya kampeni ya Chama cha Mapinduzi (CCM).”

Alichosema Katibu Mkuu Kiongozi ni kwamba Watumishi wa Umma wakiwemo Wakuu wa Mikoa na Wilaya hawaruhusiwi kutumia rasilimali za umma yakiwemo magari kwenye kampeni za kisiasa isipokuwa wanapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao  kiserikali.

Aidha, watumishi wa Umma wanaotaka kushiriki katika katika kampeni za kisiasa ama kugombea nafasi yoyote ya kisiasa sharti wajiudhulu nyazifa zao za utumishi wa umma.

Kupitia taarifa hii, Watumishi wa Umma na wa Kisiasa wanaombwa kuzipuuza taarifa hizo potofu zilizoandikwa na gazeti la Nipashe na wanashauliwa kufuata maelekezo yaliyomo kwenye Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Namba 1 wa Mwaka 2015. Walaka huu unaeleza bayana utaratibu na jinsi Watumishi wa Umma wanavyoweza kushiriki katika kugombea ama kufanya kampeni za kisiasa na utaratibu pindi mtumishi wa umma anataka kugombea nafasi ya kisiasa.
  
Imetolewa na Idara ya Habari Maelezo

13 Septemba, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...