Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akizungumza wakati wa Mkutano
wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu dhana ya wajibu wa kuwalinda
raia, ambapo alisema licha ya kuasisiwa kwa dhana hiyo dunia bado
imeendelea kushuhudia maisha ya watu wasiokuwa na hatia yakiendelea
kupotea kwa sababu tu Jumuiya ya Kimataifa inashindwa kutumiza wajibu
wake kwa wakati.
Balozi
Tuvako Manongi akizungumza wakati wa Majadiliano ya Baraza Kuu la Umoja
wa Mataifa kuhusu dhana ya kuwalinda raia (R2P) majadiliano
yaliyojielekeza katika kutathimini mafanikio na changamoto za utekelezi
wa dhana hiyo ikiwa ni miaka kumi tangu kuasisiwa kwake.
Picha hii ya maktaba ni ya wakimbizi katika kambi moja nchini
Tanzania, ambao jana jumanne akizungumza katika Mkutano wa Baraza Kuu
la Umoja wa Mataifa, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika UN Balozi
Tuvako Manongi amesema kutoka na wimbi kubwa linaloendelea la wakimbizi
kukimbilia mataifa mengine kutafuta usalama wao. Jumuiya ya kimataifa
haina budi kushirikiana na bila kubagua katika kuwalinda na utoaji wa
huduma na misaada ya kibinadamu kwa wakimbizi.
Na Mwandishi Maalum, New York
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, imetoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa wa kushirikiana
katika wajibu wa kuwalinda na kuwapatia
misaada ya kibinadamu, wakimbizi wanaokimbia
machafuko, vita na migogoro katika nchi
zao.
Wito huo umetolewa
siku ya jumanne na Balozi Tuvako Manongi,Mwakilishi
wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, wakati
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,
lilipokutana kwa majadiliano ya
siku moja kuhusu utekelezaji wa dhana juu ya wajibu wa kulinda raia
(R2P) mafanikio na changamoto zake.
Dhana ya wajibu wa kuwalinda raia dhidi ya
mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita,
mauaji ya kikabila na uhalifu dhidi ya
binadamu ilianzishwa mwaka 2005
wakati wa mkutano wa Kimataifa uliofanyika mwaka huu, ambapo viongozi
wakuu wa nchi na serikali walikubaliana kwamba wajibu
wa kwanza wa kuwalinda raia dhidi ya
udhalimu wa aina yoyote ile ni wa serikali yenyewe husika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...