Taswira ya Uwanja wa Kaitaba ulivyo kwa sasa.

Mwakilishi kutoka shirikisho la soka Duniani (FIFA) baada ya kukagua maendeleo ya uwekaji nyasi bandi katika uwanja wa mpira wa Kaitaba Amewaomba mafundi kuongeza kasi ili ukamilike kwa muda uliopangwa. Mwakilishi huyo wa FIFA Mhandisi Kelvin Macklain, alitua Bukoba wiki iliyopita na kukagua hatua kwa hatua uwanja huo na alifika hapo kukagua hatua za mwisho kabla ya nyansi husika kuanza kutandazwa, ambazo tayari zipo katika uwanja huo. 
Hata hivyo Katibu wa chama cha Soka Wilaya ya Bukoba Malick Tibabimale, alisema kuwa sehemu ya kati ya uwanja itakamilika ndani ya mwezi mmoja, na timu ya Kagera sugar itaanza kuutumia uwanja huo baada ya mechi zake nne za mzunguko wa kwanza. 
Timu ya Kagera Sugar kwa sasa itaendelea kutumia Uwanja wa Musoma kama uwanja wake wa nyumbani katika Ligi kuu ya vodacom iliyoanza kutimua vumbi jumamosi septemba 12, 2015.
Nyasi bandia zikiwa zimewekwa pembeni ya Uwanja tayari kwa kutandikwa katika Uwanja huo

Mhandisi kutoka kampuni ya Artificial Grass africa, wanaojenga uwanja huo Pierre De Groote baada ya kuukagua Uwanja huo alisema watamaliza kazi yote mwezi Desemba mwaka huu 2015.Mhandisi Kelvin Macklain Mwakilishi kutoka FIFA akifanya vipimo katika Uwanja wa Kaitaba unaoendelea kujengwa mpaka sasa. Picha zote na Faustine Ruta wa bukobasports.com
Sehemu ya katikati ya Uwanja wa Kaitaba ambayo itakamilika mwezi huu wa tisa.
Picha zote na Faustine Ruta wa bukobasports.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...